Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nianze kwanza na hoja zilizochangiwa na upande wa Upinzani, kila Wizara inayokuja hapa Wazanzibari wanataja Maalim Seif, Maalim Seif, Maalim Seif.
wananchi ili tuje tuwatetee siyo kumlilia mtu na familia yake. Ninachosikitika zaidi kuna wababa wenye jinsia kama mimi wanamlilia baba mwenzao siwaelewi.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie suala la pili, sasa hivi kumekuwa na ugumu Watanzania kupata viza za kwenda China. Ukitaka viza ya China inachukua hadi wiki tatu kuipata, ukiuliza sababu wanasema Watanzania wanafanya uhalifu China. Naomba niulize Watanzania wanaoishi China na Wachina wanaoishi Tanzania wapi wanaofanya uhalifu? Sasa hivi kuna maji feki, matunda feki, mayai feki na maziwa feki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Wachina walioko Tanzania hawafiki hata robo ya Watanzania walioko China kwa nini Wizara wa Mambo ya Nje inakubali na inasimamia unyanyasaji wa namna hii kwa Watanzania? Kila leo tunasikia wanafungwa, sisi tukiwakamata Wachina siku ya pili tunawarudisha kwao, mbona hao wanaokamatwa China hawarudishwi huku?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala hilo hilo, kupata viza ya kwenda Uingereza ni zaidi ya kwenda peponi.
Ukitaka viza ya Uingereza kuna manyanyaso sijui mpaka upate mwaliko, mbona wazungu wakija huku mnawagongea visa airport pale hamuwahoji wanakuja kufanya nini? Hiyo ni kero kubwa, naomba Waziri wa Mambo ya Nje alitolee ufafanuzi, kwa nini Watanzania tunapotaka kwenda nje tunanyanyaswa kwani sisi hatuwezi kwenda kutembea Uingereza, kwani hakuna watu wenye uwezo wa kwenda kutembea huko, mbona mnatuwekea matuta mengi tunapotaka kwenda Uingereza? Waziri naomba alisimamie suala hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanatoka nchi za nje ili mradi wawe wazungu hata nauli za kujia Tanzania wamekopa, lakini nashangaa Wizara ya Mambo ya Nje inakuja baadaye inawabadilisha wale watu wanakuwa wawekezaji. Tena wawakezaji hao wanadhaminiwa na nchi yetu wanakwenda kukopa kwenye benki zao kwa kutumia ardhi yetu huku Wizara ya Mambo ya Nje ikiwa inaangalia. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba aliangalie na suala hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la lingine ni la uraia pacha, limezungumzwa tangu nikiwa mdogo, uraia pacha, uraia pacha. Hivi kuna ugumu gani katika suala hili la uraia pacha? Naomba Mheshimwa Waziri atuambie ni madhara gani tutapata kutokana na Watanzania kuwa na uraia pacha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, limezungumziwa suala la mjusi, naona Wabunge wengi wanapiga kona. Mimi nitajitolea kama kuna ugumu wa kumsafirisha huyo mjusi kumleta Tanzania, nitakubali posho zangu zikatwe mjusi arudishwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sina mengi, hayo tu yananitosha.