Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa muda huu kupewa na mimi nafasi ya kuchangia bajeti kuu. Nianze moja kwa moja kuchangia bajeti hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nazungumzia bajeti iliyotengwa kwa vyombo ambavyo vinatakiwa kusimamia bajeti hii, taasisi simamizi, oversight institutions, kwa maana ya TAKUKURU na Ofisi ya CAG. Ni kweli wazungumzaji wengi wameongea, Ofisi ya CAG ni muhimu, ndiyo jicho, tunajua asilimia 40 imetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, lazima kuwe na jicho hili, tumuongezee pesa huyu afuatilie fedha hizi, hii shilingi bilioni 44.7 haitoshi, tunaomba aongezewe fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini TAKUKURU pia, wengi walikuwa wanasema amewekewa hela nyingi, hakuna, hela imepungua. Naomba ku-declare interest kwamba mimi nimekuwa Kamanda wa TAKUKURU - Kanda Maalum mpaka nakuja hapa. Mkoa wa Dar es Salaam kwa muda wa miaka mitano, kwa mfano 2012/2013, OC ambayo ndiyo inayotumika kwa ajili ya mafuta watu waweze kwenda kufanya kazi, ndiyo kuna per diem za watu zipo hapo ili waende kufanya kazi, ndiyo kuna fedha za stationeries kwa ajili ya kwenda kufanya kazi ilikuwa shilingi bilioni 16, mwaka 2013/2014 ilikuwa shilingi bilioni 15.5, mwaka 2014/2015 ilikuwa shilingi bilioni 16.5, mwaka 2015/2016 ilikuwa shilingi bilioni 14.2 ikapungua, mwaka huu wa fedha 2016/2017 ni shilingi bilioni 12.03, imepungua sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia hii 40 inakwenda kwenye miradi, watu mambo yameongezeka lakini pia taasisi hii watu wamekuwa wengi, wapo wafanyakazi karibu 2,001, magari yameongezeka, mafuta yanahitajika lakini tunayo shilingi bilioni 12 tu. Kipindi kile kabla sijastaafu kule tulikuwa tunajibana sana kwa hizi shilingi bilioni 16, 15, 16, 14, sasa mwaka huu hata fedha yenyewe imeshuka wanakuja kwenye shilingi bilioni 12 yaani hii hela ni ndogo mno, sijui, namhurumia sana huyu Mkuu wa TAKUKURU sijui atafanya kazi gani. Atafanya lakini kwa kujinyima na hali kwa kweli ni ngumu sana, wanategemea kufungua wilaya nyingine 25, wana-operate mikoa yote, wilaya zote za zamani, sijui watafanya nini.
Mheshimiwa Naibu Spika, rushwa ndugu zangu ni adui wa haki, rushwa tunaona madhara yake ni makubwa mno, taasisi hii iko kila mahali. Rushwa imesababisha migogoro ya ardhi, ni kazi ya ofisi hii, rushwa imeingia michezoni watu wanapnga matokeo ni kazi ya taasisi hii, rushwa imeingia hospitalini, twende mahakamani watu wanabambikiwa kesi vituo vya polisi ni kazi ya ofisi hii, wakandarasi tunapata wabovu yaani kuna vurugu. Nenda sekta ya ardhi akina mama wanadhalilishwa, rushwa ya ngono, ajira, ni kazi ya TAKUKURU kwenda kule. CAG ni moja wa informers wa TAKUKURU, makabrasha yale yote yanashughulikiwa na ofisi moja tu. Bado nchi nzima wanapeleka taarifa TAKUKURU, atafanyaje kazi huyu?
Mheshimiwa Naibu Spika, najua hii haiwezi kubadilishwa lakini kipindi kijacho naomba suala hili litazamwe upya. Najua Watanzania wanajua hizi hela zilivyotajwa 72.3 labda ni nyingi, hapana, siyo nyingi, kuna mambo ya mishahara ile ni fixed, kuna ujenzi wa Ofisi ya Ushauri ya Afrika kule Arusha, ndiyo imeweka amount hii imekuwa kubwa lakini zile za kufanyia kazi ni ndogo mno na kwa kiasi ambacho kimepunguzwa sana mwaka huu, nawahurumia sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba taasisi hii ndugu zangu hebu tuisemee, tuitetee, ndiyo mkombozi wetu huyu. Nchi imechanwachanwa vipandevipande kwa sababu ya rushwa. Tunasimika viongozi wabovu kwa sababu ya rushwa, tuimarishe hiki chombo kifanye kazi vizuri. Yapo mambo mengi ambayo chombo hiki kinafanya inabidi tukisemee, ndiyo mkombozi wetu katika nchi hii yaani chombo hiki kikilegalega ambacho ndiyo msimamizi wa mapambano haya hali itakuwa ngumu sana. Hata uchumi wa viwanda tunaouzungumzia sijui tutakwendaje kama hatujaimarisha taasisi hii. Kwa hiyo, tuzisemee taasisi mbili hizi simamizi CAG na TAKUKURU, hawa ni mapacha, lazima tuwatetee, wapewe fungu kubwa hawa ili wafanye kazi. Nilitaka niseme hilo kwa uchungu mkubwa kwa sababu naitazama Tanzania yangu nakata tamaa kwa sababu hivyo vyombo vimepewa hela kidogo sana vitasimamiaje majukumu yao?
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kidogo property tax, kuna ugomvi hapa kidogo, TRA ni wataalam wenyewe wa mambo ya kodi, ni mahiri kwenye mambo ya kodi lakini pia Halmashauri kuna wataalam wa mambo ya ardhi, wathamini wanaojua thamani za ardhi. Kodi hii huwa ina-base kwenye thamani ya jengo pamoja na ardhi, TRA siyo wataalam wa mambo ya ardhi, wataalam wako kwenye Halmashauri, kwa hiyo kuna mambo mawili hapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nashauri, acheni wataalam wa ardhi wafanye makadirio ya kodi hii, wakabidhini sasa hawa mahiri wa kukusanya kodi maana wao ni kukusanya tu siyo kukadiria. Ndiyo maana kuna mchangiaji mmoja amesema inafika mahali sasa mnatoza flat rate, kibanda cha jiko kinakuwa na kodi yake, nyumba kubwa inakuwa na kodi yake, kwenye evaluation hatufanyi hivyo wataalam wa ardhi. Jengo moja linakuwa na vijengo vidogovidogo, vinaitwa art building, ni sehemu ya jengo kubwa, wataalam wanajua, waachieni wataalam wakadirie kodi hii, TRA wenyewe ni wataalam wa kukusanya tu, basi. Naomba hili Mheshimiwa Waziri alizingatie sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie Singida, Mkoa wangu ninaoupenda. Nimesoma hiki kijitabu kidogo kinachozungumzia hali ya uchumi, ukurasa wa 10, Singida ni namba nne kwa umaskini katika nchi hii. Jamani hatukujitakia, tumejikuta tuko pale Singida, tumezaliwa pale, ndiyo mkoa wetu sisi. Ndiyo mkoa wetu uleā€¦
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana.