Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii ya kuchangia. Ninayo mambo manne na mambo yenyewe ni mafupi mafupi tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, Sera ya Mambo Nje inabidi ifanyiwe marekebisho, tunajua ni ya mwaka 2001 kwa sababu sera ndiyo inatoa mwelekeo, tunakoelekea, inaweka priority zetu, hilo ni jambo la muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, tunasema mtengamano, fursa zilizopo, tumepata machapisho mengi, lakini ni jambo la ajabu hata sisi Wabunge tunauliza, hatujaujua sawasawa huu mtangamano. Sasa ni wakati muafaka wenzetu hawa wakachukuwa hatua za makusudi kuwaelimisha jamii inayozunguka, watu walioko mipakani waelimishwe na sisi Wabunge tuelimishwe ili tuweze kutumia fursa hizo. Kwa sababu fursa hizi zinafahamika tu kwa Wabunge wa Afrika Mashariki, zinafahamika na baadhi ya watu tu, lakini Mwananchi wa kawaida; katika nchi yetu tuna utaratibu wa utawala, tuna wenyeviti wa vitongoji, tuna wenyeviti wa vijiji wanaweza wakatumiwa hasa mipakani kuhakikisha kwamba, elimu hii inawafikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la Diaspora limezungumziwa sana, watu walioko huko. Mimi najua kwamba, iko diaspora, kuna forum ya diaspora na huwa wanakusanyika wanatambuana katika nchi mbalimbali wanazoishi licha ya mchango wanaopaswa kuuleta huku kwetu, lakini pia wao wanatakiwa kutambuana. Ni ukweli usiopingika kwamba watu wengi wamekwenda kule wamejilipua, hawatambuliki katika Balozi zetu, kama hautambuliki katika Balozi zetu zilizoko huko, utapataje huduma hiyo? Kwa hiyo, ni wakati muafaka sasa waliojificha huko watoe taarifa kwenye Balozi ili waweze kupata huduma zinazohitajika badala ya kuendelea kulalamika tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine limezungumziwa hapa, suala la Rais kusafiri nje ya nchi; kuna leadership style, leadership style ni muhimu, kiongozi anaweza akawa anasafiri nje na ikawa sawa lakini yuko kiongozi mwingine, yuko anafanya strategic planning nyumbani. maadamu nchi inakwenda, inasonga mbele na tunaona matokeo, kama tunaona matokeo hana sababu ya kusafiri. Atasafiri itakapo kuwa ni lazima, huo ni utaratibu wa uendeshaji wa nchi yake. Hata wenzetu hawa wakipata nchi watapanga utaratibu wao wa kuendesha nchi, huu ndiyo utaratibu unaoonekana ni utaratibu bora. Kwa hiyo, inabidi tuheshimu utaratibu huo, tuone nchi inaendeshwaje na sisi Wabunge hapa tushauri ili tuweze kuona kwamba tunatoa mchango katika uendeshaji wa nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Mabalozi; suala la Balozi kuzuiwa, limesemwa wanazuiwa kuwasiliana na maeneo mbalimbali, amesama msemaji wao mmoja. Uko utaratibu, hapa ni Tanzania na hapa ni kwetu na sisi ndiyo Watanzania. Balozi hawezi kuja hapa akafanya mambo anavyotaka yeye, lazima Balozi akija hapa anakuwa Monitored na asipofuata taratibu hizo tunamchukulia hatua na tunaweza kumrudisha alikotoka. Na hii imeshaonekana ni practice World Wide, inafanyika na sisi hatuwezi kwenda tofauti na hivyo. Lazima tuilinde nchi yetu, lazima tuwe na uchungu wa nchi yetu, tuweze kuona kwamba Taifa letu linakuwa salama na hao Mabalozi wanafanya kazi walizotumwa sio wanafanya kazi, ambazo wanafikiria wao kichwani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja, ya kwangu yalikuwa ni hayo machache tu, asante.