Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana, kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia siku ya leo. Lakini vilevile nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje kwa kazi nzuri ambayo anaifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niwapongeze watendaji wake wote wa Wizara hii ya Mambo ya Nje na vilevile, nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri, ambayo anaifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niwapongeze Mabalozi wetu kwa kazi nzuri, ambayo wanaifanya wakiwa katika kazi zao huko nje. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana, Mabalozi wetu walioko nje, hawa Mabalozi wetu wa Tanzania, wafanye kazi nzuri, tuwatumie katika kazi ya kutangaza utalii wetu tukiwatumia Mabalozi hawa katika kazi ya kutangaza utalii na kazi ya kutafuta Wawekezaji katika nchi yetu, basi naamini hata sekta ya utalii katika nchi yetu hii itakua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tunaamini katika sekta ya utalii ikikua, basi ni chanzo cha uchumi wetu kukua, kwa kuwa, tunaamini uchumi wetu, hii sekta ya utalii inachangia asilimia kubwa katika suala kuongezeka uchumi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namuomba sana Mheshimiwa Waziri tufanye kazi ya ziada tuhamasishe Mabalozi wetu na tuwaambie Mabalozi wetu wahakikishe kwamba wanatangaza utalii wetu wa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatembelea Balozi za wenzetu, basi ni kazi kubwa wanayoifanya, unapofika Mheshimiwa Waziri jambo la kwanza wanakuonyesha utalii wa nchi za zao. Kwa hiyo, nakuomba sana Mheshimiwa Waziri tuweze kufanya kazi hizi na Balozi zetu ziweze kufanya kazi hizi kwa maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kufanya Mabalozi wetu tunawapenda sana. Vilevile wahamasishe katika kuwatafuta wawekezaji ili kuhakikisha kwamba, nchi yetu inatumia njia hii ya Mabalozi. Sio Mabalozi hawa kuwepo kule, ikawa ndiyo imemaliza kazi tu. Tunawatumia Mabalozi wetu kuhakikisha kama wanahangaika na kazi ya kuwatafuta wawekezaji ili nchi yetu ipate maendeleo kwa kuwatumia Mabalozi hawa, tusiwe na Mabalozi tumewaweka tu wakati kazi haifanyiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe sana Mabalozi hawa wafanye kazi ya ziada ili wafahamu kwamba nchi yetu tukiwapeleka kule na sisi tunawategemea kwa hali na mali, tunawategemea wafanye kazi kwa huruma zao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, jambo kubwa linasikitisha sana hili. Jambo la makazi, jambo la majengo ya ofisi za Balozi zetu, hizi hali zimekuwa mbaya, haziridhishi kabisa haya majengo. Mabalozi wetu na watendaji wetu, wanafanya kazi katika wakati mgumu, na wanakaa pahala pabaya, zinafika hatua hata nyumba nyingine, zinafika hatua ya kuvuja na tukitegemea majengo haya yatafika hatua ya kuporomoka tutapata hasara kubwa katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nigusie suala la watendaji wetu. Watendaji wetu katika sekta hii, jambo kubwa sana wanatakiwa wapewe mafunzo ya kutosha. Inaonekana wafanyakazi wetu, watendaji wetu bado mafunzo yetu katika ufanyaji wao wakazi, umekuwa uko duni sana. Naiomba Wizara yako, naamini Waziri wewe ni msikivu utafanya hii kazi, hawa wafanyakazi wetu waweze kupata mafunzo bora. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa wafanyakazi wanapopata mafunzo ya uhakika, basi hata utendaji wao wa kazi, utakuwa wa kuboresha sana katika kazi hii ya kutangaza utalii wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyakazi wetu tukiwapeleka wanakuwa kama si wafanyakazi tofauti na Balozi wa nchi za wenzetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.