Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa fursa nichangie Wizara hii ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote ninampongeza sana mwanamke wa kwanza katika historia ya Tanzania ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais, mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu. Licha ya kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais mwanamke, lakini vile vile Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amemteua kuwa kwenye jopo la juu kabisa la ushauri jinsi gani ya kuweza kumuwezesha mwanamke. Ninaamini kwa njia hii wanawake wa Tanzania tutanufaika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo mimi naomba nianze yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni sovereign state, lakini cha ajabu ukiangalia nchi kama Israel, Australia, Uingereza, Canada masuala yote ya viza unapoyahitaji hayapatikani hapa Tanzania. Sasa nilikuwa nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri, shemeji yangu, ninayemuheshimu sana, suala la bilateral limefikia hatua gani mpaka visa hazitolewi hapa nchini kwetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni suala zima la diplomasia ya kiuchumi. Foreign Minister wa Australia by then Julie Bishop aliwahi kusema, just as traditional diplomacy aims for peace and security, so economic diplomacy aims for prosperity. Kwa nini ninasema haya? Hii diplomasia ya kiuchumi ilianza nchini kwetu mwaka 2001, lakini nilikuwa nahitaji sana Mheshimiwa Waziri atuambie, as of to date, sera hii ya kiuchumi imefikiwa vipi na imefanikiwaje na tumei-utilize namna gani kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge Masele pale, maana hii economic diplomacy ndiyo injini ya sasa hivi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaelewa kuna changamoto za pesa, lakini kuna suala zima la commercial attaché, niliwahi kuuliza hapa swali, tatizo la commercial attachés wetu kazi zao hazionekani vizuri na wengine wako inactive ama hawapo kabisa kwenye Balozi zetu. Lakini ajabu nikajibiwa kwamba Wizara hii ni mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapozungumzia economic diplomacy kwa misingi hii sijui ni nini kifanyike. Ushauri wangu kwa Serikali, ni kama huu ufuatao; pamoja na kwamba diplomacy is expensive but in order to move tunatakiwa tufanye nini? La kwanza tunatakiwa tuwe na various capacity building kwa foreign staff wetu ili waweze kujua wanaweza wakaitangaza nchi yetu namna gani kule nchi za nje pamoja na vivutio vyake. Na hawa ndugu zetu ma-foreign staff wanatakiwa pia wawe ma-lobbyists wazuri, wawe negotiators wazuri, wawe smart, waweze ku-strategize waweze kuwa innovative. Na ndiyo maana ninazungumzia tuweze kuwa na capacity building za mara kwa mara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile performance appraisal inatakiwea kufanyika, wapewe marbles, wapewe goals ili tuweze kuwa na deliverables ziweze kuonekana, vinginevyo tutakuwa tunafanya business as usual. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika hizi Balozi zetu tunatakiwa tuwe na tourists experts kama wale wa uhamiaji wanaoshughulikia viza. Lakini hawa tourists experts wetu ambao tunakiwa tuwe nao katika zile Balozi zetu na wenyewe wajaribu kuwa strategists, kwa maana ya kwamba wawe katika zile nchi ambazo tunaweza tukafanya ubalozi wetu na biashara ya utalii kwa vizuri. Kwa mfano, nchi ya China sasa hivi wote ni mashahidi, ni nchi ambayo inakua kwa kasi na vilevile inaweza ikaleta ndege tukawa na uwekezaji; ukizingatia pia Watanzania wengi wanafanya biashara kule China, na vilevile tukaweza kuwa na consulate pale Guangzhou na tukafanya utaratibu wa Watanzania hawa kuweza kuwa na partnership pamoja na wale wenzetu wa China.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ni suala zima la shuttle diplomacy. Katika Bunge lililopita jambo hili nililizungumzia sana. Ninatoka Mkoa wa Mbeya, Mkoa wa Mbeya kuna Ziwa Nyasa na tunajua upande wa Ziwa Nyasa kuna suala zima la Heligoland, maana hii ni tangu enzi za Kamuzu Banda. Lakini Mheshimiwa Waziri hapa kwenye taarifa yake hajazungumzia mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa mpaka leo hii imekuwa vipi. Sisi tunaotoka katika Ziwa Nyasa na wenzangu wengine wote tungependa kujua mpaka leo hii suala hili llimefikia wapi na suala zima za shuttle diplomacy limefikia wapi kwa sababu wakati ule Mzee wetu Chissano na wenzake walikuwa wanajaribu kulizungumzia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala zima la conference diplomacy. Hii ninajua ina gharama zake na sasa hivi tunajua wengi hawasafiri sana na ndiyo maana nikazungumzia masuala ya foreign staff wapewe ile capacity building, lakini vilevile katika suala zima la bilateral na multilateral basi tujaribu kuangalia sana kama tunaweza tukawa na forums za aina mbalimbali kuweza kufanyika hapa nchini kwetu ili tuweze kuongeza Pato la Taifa, tuweze kutangaza nchi na vivutio vyake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni majengo yetu katika Balozi zetu. Waheshimiwa wengi hapa wamezungumzia, ukweli majengo yetu katika balozi yanatia aibu sana, hakuna fedha. Sasa tufanyeje ili majengo haya yaweze kufanyika katika njia itakayokuwa bora na ya ufanisi? Kwanza yanatakiwa kukarabatiwa; ama tuweze kujenga majengo ya staff wetu, vinginevyo tusipoangalia gharama zitakuwa ni kubwa sana zile za kupangisha. Kwa maana hiyo tujenge balozi zetu, vile vile tuimarishe au tuboreshe makazi ya staff maana na wenyewe wanakuwa hawana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo mawazo yangu kwa leo yalikuwa ni machache, nisingependa nigongewe kengele, ninaunga mkono hoja, ahsante sana.