Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwanza nataka Watanzania ambao wanatusikiliza waelewe kwamba sisi kama Kambi ya Upinzani tutaendelea kushikilia misimamo yetu dhidi ya ukandamizaji wa demokrasia na sisi tuko makini kweli kweli, hiyo ya kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wakati alipokuwa akitoa hotuba yake alisema miongoni mwa taasisi ambazo anaziongoza tatu ni APRM (African Peer Review Mechanism) mpango ni wa kujitathmini wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa huu mpango Tanzania inajitathmini yenyewe ningependa nimuulize Mheshimiwa Waziri atueleze, kwa sababu huu ni mpango wa utawala bora, huu mpango wa Bunge kutooneshwa live mmejitathmini kiasi gani? Mpango huu wa Bunge kutooneshwa live ni kiasi gani mmejitathmini ninyi wenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, viongozi wetu kukatwa katwa mapanga na kupigwa na kuumizwa na wengine kuuawa kama kwa kamanda Alphonce Mawazo ambaye yeye ni Mwenyekiti wa Mkoa wa CHADEMA, kiasi gani mmejitathmini na nani waliohusika katika mpango huu wa utawala bora? Pia sambamba na hilo ningependa kuelewa kupigwa na kukatwa katwa na kuuawa kwa Diwani wetu kule Muleba, Faustine Mlinga, Kata ya Kimwani, kiasi gani mmejitathmini na kujua nini cha kufanya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuelewa kuvamiwa kwa viongozi mbalimbali wa dini kule Mwanza juzi na kupigwa. Je, katika mfumo huu wa utawala bora ni kiasi gani mmejitathmini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuuawa kwa vikongwe, walemavu, wale albinism, kiasi gani mpango huu wa kujitathmini wenyewe mmeweza kukaa kitako na mkaona njia gani mbadala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema haya ili tuelewe sasa kiasi gani APRM, kwa sababu haina vote yake yenyewe hampewi fedha, kwa hivyo sasa ionekane kiasi gani katika kujitathmini ninyi wenyewe kama uwezo wenu ni mdogo, hamna fedha, mimi naishauri Serikali, APRM (African Pear Review Mechanism) ipewe vote yake yenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuna masikitiko makubwa, Watanzania ambao wanataka kwenda Uingereza viza zao zamani walikuwa wanazipata Kenya, sasa mpaka Afrika ya Kusini. Mheshimiwa Waziri, tuambie tatizo gani la figisu figisu baina ya Tanzania kutoaminiwa na Uingereza mpaka viza hizi kutoka sasa kwenda kutoa Kenya sasa unazipata Afrika ya Kusini, tatizo ni nini? Mna tatizo gani la kidiplomasia na hawa wenzetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ni diplomasia ya kiuchumi. Nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri ingawa anaongea ongea pale, katika kuongeza kasi hii ya diplomasia ya kiuchumi baadhi ya nchi zimeweza ku-present credentials, kupeleka hati za utambulisho hapa kwetu, na sisi inaonekana bado kuna nchi mbalimbali hatujaweza kuwasilisha hati za utambulisho. Tanzania hapa Balozi wa Namibia na Botswana wako Tanzania lakini sisi Balozi wetu kule Botswana na Namibia naona kama sisi hatuna Balozi.
Lakini tarehe 05 Januari, 2016 kuna nchi tatu ambazo waliweza ku-present credentials hapa. Jamhuri ya Korea, Jumuiya ya Ulaya na Taifa la Palestina. Je, sisi tumejipanga vipi? Wakati wao tarehe tano walileta hiyo hati ya utambulisho kwa Rais John Pombe Magufuli, sisi je, kwa nchi ambazo nimezitaja. Jamhuri ya Watu wa Korea, Jumuiya ya Ulaya na Taifa la Palestina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba Mheshimiwa Waziri ukija unieleze, ni kwa nini sisi tunachelewa kuwasilisha hati za utambulisho? Mfano Balozi wetu pale Berlin, Ujerumani, nchi ambazo anaziwakilisha ni Ujerumani, Uswiss, Jamhuri ya Czechoslovakia, Poland, Hungary, Bulgaria, Romania, Australia na Vatican, lakini hati ambazo zimewasilishwa na Ujerumani, Uswiss, Austria na Vatican, nyingine zote mpaka leo hatujawasilisha hati za utambulisho, tatizo ni nini na hii ni diplomasia ya kiuchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo Cairo, pale Misri Balozi wetu nchi ambazo anaziwakilisha ni Misri, Israel, Lebanon, Palestina, Libya, Iraq, Syria na Jordan. Lakini hati ambazo zimewasilishwa ni Misri peke yake, nyingine zote bado hatujawasilisha hati za utambulisho na hapa uchumi wetu utakuwa ukiendelea kudorora siku hadi siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba Mheshimiwa Waziri, utakapokuja uniambie…
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Masoud, dakika tano zako zimekwisha.