Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SILAFU JUMBE MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza jitihada ya kazi nzito ifanyikayo katika kuendeleza, kuilinda na kujenga hasa mahusiano nchi za nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki. Waziri na jopo lake kwa kazi yenye matumaini kwa nchi yetu ya uchumi wa viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema Serikali kuona upya namna ya kujipanga na kuweka bajeti yenye tija hasa katika kuwezesha ujenzi wa mahusiano wa nchi za nje, kwa kupata wataalam wa kuwajengea uwezo vijana wetu na kusimama wenyewe na hata upatikanaji wa Wawekezaji mahiri ambao wakitumia malighafi zilizopo na wanapoondoka viwanda vyetu kuendelea kuzalisha, yaani tuweze kubakiwa na viwanda mama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kuona umuhimu wa kuweka msukumo wa kusimamia ongezeko la bajeti kuwezesha nchi yetu kupiga hatua sasa ya kuwajenga vijana wetu, kwa kukiwezesha Chuo cha Kidiplomasia kwa kuongeza idadi ya udahili, tukifahamu kuwa chuo hiki Tanzania ni kimoja tu hivyo kipanuliwe au kuwa na branch kwa upande wa Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ofisi za Mabalozi wetu huko nje, kuendelea kupanga na makazi ya Mabalozi, ni suala la kuangaliwa upya, madamu tunazo Taasisi na Mifuko ya Jamii inaonesha uwezo wa ujenzi wa majengo makubwa,
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
222
kwani hawawezi kupewa ukandarasi wa ujenzi wa majengo hayo. Ni lini sasa Serikali itayafanyia kazi na kuondokana na utaratibu wa upangaji huko nje, kwani wao kwetu wanajenga?
Mheshimiwa Spika, utaratibu wa wananchi katika kusafiri kwenda nchi za nje, kuna urasimu sana, kuliko wanaoingia nchini na sasa idadi yao inatisha na wote wanakuwa ni wafanyabiashara na wawekezaji na baadhi yao kuwa wahalifu nchini. Serikali inalazimika kuongeza nguvu zaidi ya kiusalama katika maeneo yote na kudhibiti hii hali ya mwingiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.