Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi lakini nasikitika naenda kuchangia wakati Waziri mwenyewe hayupo; kwa sababu ilibidi hivi vitu avibebe Mheshimiwa Waziri yeye mwenyewe ndio tungeenda sawa zaidi, lakini sio mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na kuna Wabunge wapya humu wanashangaa suala la sisi kutoka Bungeni sijui tunasaini, sijui tunafanya nini; niwataarifu tu wanatakiwa kabla hujaingia kwenye kitu upate elimu kuhusu utendaji wa hicho chombo au taasisi. Kutoka Bungeni ni suala la kawaida kabisa kwa sababu hata tunavyotoka sio kwamba tunatoka tunakwenda nyumbani; kwa sababu kuna wakati ni heri uwe nje unatumia simu kuongea na watu Jimboni kuliko kukaa humu ndani kusikia watu wanavyo zomea zomea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na niwataarifu tu kwamba tutaendelea kutoka hatua hii mpaka pale kiti anapokaa Naibu Spika aache tendency za udikteta ndani ya Bunge kwa sababu tupo humu tunataka freedom kwa ajili ya masuala yanayohusu hili Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la diplomasia, Wizara hii ni muhimu sana na imefika mahali tunatakiwa tuweke mbele diplomasia ya uchumi; naongea hivi nikiunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Msigwa, Waziri Kivuli kwa sababu tunatakiwa tutoke sasa tuachane na diplomasia ya enzi za cold war. Diplomasia hiyo imepitwa na wakati, lakini unfortunately sisi ndio tunabaki nayo na afadhali hata zamani tulikuwa na misimamo. Sasa hivi hata misimamo hatuna, Wizara ya Mambo ya Nje kazi yake ni pamoja na kusimamia, kuwa MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi lakini nasikitika naenda kuchangia wakati Waziri mwenyewe hayupo; kwa sababu ilibidi hivi vitu avibebe Mheshimiwa Waziri yeye mwenyewe ndio tungeenda sawa zaidi, lakini sio mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na kuna Wabunge wapya humu wanashangaa suala la sisi kutoka Bungeni sijui tunasaini, sijui tunafanya nini; niwataarifu tu wanatakiwa kabla hujaingia kwenye kitu upate elimu kuhusu utendaji wa hicho chombo au taasisi. Kutoka Bungeni ni suala la kawaida kabisa kwa sababu hata tunavyotoka sio kwamba tunatoka tunakwenda nyumbani; kwa sababu kuna wakati ni heri uwe nje unatumia simu kuongea na watu Jimboni kuliko kukaa humu ndani kusikia watu wanavyo zomea zomea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na niwataarifu tu kwamba tutaendelea kutoka hatua hii mpaka pale kiti anapokaa Naibu Spika aache tendency za udikteta ndani ya Bunge kwa sababu tupo humu tunataka freedom kwa ajili ya masuala yanayohusu hili Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la diplomasia, Wizara hii ni muhimu sana na imefika mahali tunatakiwa tuweke mbele diplomasia ya uchumi; naongea hivi nikiunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Msigwa, Waziri Kivuli kwa sababu tunatakiwa tutoke sasa tuachane na diplomasia ya enzi za cold war. Diplomasia hiyo imepitwa na wakati, lakini unfortunately sisi ndio tunabaki nayo na afadhali hata zamani tulikuwa na misimamo. Sasa hivi hata misimamo hatuna, Wizara ya Mambo ya Nje kazi yake ni pamoja na kusimamia, kuwa Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ndio diplomasia inayotakiwa kufanyika sasa hivi lakini hatuna rekodi; angalia kama Ethiopia wanavyojaribu kuwashirikisha diaspora yao katika masuala ya uchumi. Walianzisha mradi mkubwa sana wa umeme pale unaitwa Ethiopian Grand Millennium Dam kutokana na mgogoro wa chanzo Nile na support inayopata Egypt baadhi ya mataifa wakakataa kui-support Ethiopia kifedha kwenye ule mradi; walichofanya Serikali ya Ethiopia wakawahusisha watu wao wa diaspora Worldwide, wakawatengenezea bond maalum, wakawawekea utaratibu wale mabwana wanachangia sasa dola kwenye ule mfuko na Ethiopia sasa hivi ule mradi nilikuwa naangalia jana umefikia asilimia 70 ya kutengenezwa, wamebaki asilimia 30 tu kutengeneza bila fedha za nje kwa kutumia fedha za diaspora ya Ethiopia inayoishi North America na Uingereza ndugu zangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sasa sisi tumekaa tu Ethiopia wanatumia diaspora wanakwenda kuwa na bwawa kubwa, wanaenda kutengeneza historia, wana bwawa kubwa la umeme kuliko yote Afrika kwa kutumia diaspora. Sisi diaspora hatuwashirikishi; huwezi kuwashirikisha watu kwenye uchumi; Watanzania hawa huwezi kuwashirikisha kwenye uchumi wakati hautaki kutambua uraia wao, uzalendo wao na utaifa wao. Hapa nazungumzia diaspora maana yake tunafika mahali tunachanganya mambo, ninyi mnachanganya kati ya utaifa na uraia. Utaifa ni kitu natural, uraia ni kitu cha documentation yaani paper work, kama mimi ningeamua kufanya paper work sasa hivi ningekuwa raia wa Marekani, lakini utaifa ni kitu by nature.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hatuwezi kwenda mbele bila kuwashirikisha hawa watu; mnawadanganya watu mnaenda mnawaambia rudini nyumbani wakirudi nyumbani hawawezi kuacha mambo yao waliyoyatengeneza kule miaka yote eti aache uraia wa Marekani aje hapa akitaka kibali hichi corruption, akitaka hichi corruption na pia aje kama mgeni. Anatakiwa mnatambua mnawapa dual citizenship ili wanavyokuja hapa wanakuja kama Watanzania sio Mtanzania yupo Marekani mmemnyang‟anya utaifa wake kwa sababu ya makaratasi ya uraia halafu anakuja hapa mnamzuia kabisa mnataka awe mwekezaji kama mgeni na sio kama Mtanzania wa hapa, sasa hii ni mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi kwa nini mnaogopa sana diaspora, kwa nini mnaogopa sana dual citizenship mnajua ni hasara kiasi gani mnalipa hili Taifa kwa kutokujua tu remittances zinaingizwa nchini kiasi gani hiyo ni upungufu mkubwa sana na tunaitaka hii Serikali sasa hivi ifanye mkakati walete dual citizenship ili watanzania waliopo nje walete input na sio tu input ya kiuchumi exposure waliyoipata wale mabwana kule hata katika masuala ya utawala tukiwaleta na kuwaingiza katika mfumo wa uendeshaji nchi hivi vitu vidogo vidogo vya uzembe uzembe, rushwa rushwa ndogo ndogo hizi havitakuwepo kwa sababu good governance itaenda kutamalaki pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sisi tumekaa, Serikali haiwajali diaspora wakiwa hai na hata wakiwa wamekufa; Watanzania wanauwawa huko kama niki-refer hotuba ya Waziri Kivuli, niende kwenye mauaji ya juzi juzi tu Watanzania wawili katika mwezi mmoja mwezi wa nne wamepigwa risasi hakuna tamko lolote mpaka tupige kelele Bungeni humu ndio Waziri atakuja baadaye atajifanya anatoa tamko wakati alitakiwa walishughulikie hili suala na naunga mkono petition ya Watanzania wanaoishi Marekani ambao wanataka Balozi wa Marekani Washington DC aondolewe mara moja arudishe nyumbani kwa sababu ameshindwa kuwatumikia Watanzania kule Marekani. Ameshindwa kutambua hata pole hajatoa kwenye misiba hii iliyotokea. Umetokea msiba wa Andrew Sanga, Afrika nzima imelia; Serikali haina habari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Andrew Sanga amepigwa risasi amekufa Serikali hii haina habari; Balozi wa Marekani anapigiwa simu kuna msiba Houston ameacha kwenda kwenye msiba Houston anasema nina udhuru, udhuru wenyewe yupo Dallas, Dallas na Houston ni kama Dar es salaam na Morogoro. Amekwenda Dallas kwenye party ameacha kwenda kwenye msiba ambao umetingisha Marekani nzima na yeye angeenda pale angeenda kuleta harmony kidogo na kuwatuliza wale watu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka Waziri atuambie na aliambie Bunge lako Tukufu Serikali hii imefikia wapi kufuatilia uchunguzi wa mauaji ya Andrew Sanga kwa sababu Marekani usipo-push na wao wana-relax kwa sababu wanajua…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi muda umemalizika naomba ukae.