Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hii Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Kabla sijaanza kuchangia naomba nijikite moja kwa moja, kwenye Mkoa wetu wa Simiyu, ukiwemo na wewe mwenyewe Mwenyekiti, nadhani nikiutaja Mkoa wa Simiyu hata nisipozungumza chochote naamini roho yako inakuwa burudani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikiongoza kupata chakula kwa wingi, lakini kwa kipindi hiki mkoa huu umekuwa ukiongoza kwa janga la njaa. Unaongoza kwa janga la njaa kutokana na kwamba wananchi wa Mkoa wa Simiyu wamekuwa wakitegemea kilimo cha msimu badala ya kutegemea kilimo cha umwagiliaji. Hivyo basi, kuliko wananchi hawa waendelee kutegemea kilimo cha msimu, naomba wananchi hawa wategemee kilimo cha umwagiliaji ili waondokane na janga la njaa ambalo linatukabili kila mwaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili wananchi hawa waondokane na njaa ni lazima Serikali itengeneze miundombinu ya kututengenezea mabwawa kwa maana ya kuendesha kilimo cha umwagiliaji. Baada ya kututengenezea mabwawa hayo, naamini kabisa kwamba Mkoa wa Simiyu utakuwa umekidhi matatizo ya njaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa ambayo imezungukwa na Ziwa Victoria, lakini ni Mkoa ambao ndiyo unaoongoza kwa ukosekanaji wa maji. Naomba nizungumzie kwa mfano Wilaya ya Busega Jimbo la Mheshimiwa Chegeni. Wananchi wa Wilaya ya Busega, walio wengi wanaoga maji ya kutoka Ziwa Victoria. Cha kushangaza wananchi hawa wanakunywa maji ya chumvi ya visima, ni jambo ambalo ni la kusikitisha na ni la aibu kwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka kwa Bunge lililopita niliuliza swali kuhusiana na suala la utekelezaji wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuwapatia maji safi na salama wananchi wa Mkoa wa Simiyu. Nilijibiwa kuwa mpango huu, unaendelea na hivi punde mradi utakamilika, lakini mpaka ninavyoongea hakuna kinachoendelea tunaendelea kupata takwimu tu na taarifa za kwamba mradi huu utakamilika jambo ambalo naona kwamba siyo sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Simiyu kuna Idara za Maji, siku zote nimekuwa najiuliza kwamba hivi Idara za Maji zinafanya kazi gani, ilihali wananchi wa Mkoa wa Simiyu hawana maji, maji ambayo tumekuwa tukiyatumia wananchi wanatengeneza makazi yao na wanachimba visima kwenye majumba yao na wanakuwa wanatumia na walio wengi unakuta wanafanya biashara ndoo moja shilingi mia mbili, lakini unakuta kuna Wizara ya Maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kupata majibu kwamba hii Wizara ya Maji inafanya kazi gani, ambapo wananchi wa Mkoa wa Simiyu hatuna maji. Kiukweli tunapozungumza kuhusu maji ni dhahiri kweli tunapata uchungu kutokana na kwamba Mkoa huu wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa ambayo ni mipya, lakini kiukweli mara nyingi umekuwa unasahaulika hata kutajwa kwenye Wizara zingine. Sijajua kwamba hatima ya Mkoa huu wa Simiyu ni nini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia hapa kwenye kitabu chake ametutengea fedha Wilaya ya Itilima ambayo mimi natoka na ni Mwenyekiti wa chama katika Wilaya hiyo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), nimekuta wametenga shilingi milioni 200 ni sawa, lakini nimeona Wilaya ya Busega hakuna fedha ambazo zimetengwa kutekeleza mradi huu wa maji. Pia katika Jimbo la Mheshimiwa Mwenyekiti pale Bariadi sijaona fedha ambayo imetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa maji, nimeona Jimbo la Maswa hakuna fedha yoyote ambayo imetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sijajua huu mpango unakwenda vipi, kwa sababu fedha nilizoziona pale Wilaya ya Itilima inayo, Wilaya ya Mwanuzi ipo, ni wilaya kama mbili hivi. Kwa hiyo, sasa nashindwa kuelewa kwamba huu mradi unakwenda kutekelezwa vipi? Hii inaonesha wazi kwamba jinsi ambavyo pamoja na kwamba tunatoa hizi taarifa, ijulikane kabisa kwamba sidhani kama kuna mpango wowote unakwenda kutekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna mpango unakwenda kutekelezwa, ni dhahiri basi tuanzie pale kwenye vyanzo vya maji, kwa mfano Wilaya ya Busega, ndiyo iko karibu sana na ziwa, kwa nini hatujaona mpango wowote wa kutoka pale Busega, lakini pia Bariadi ndiyo inayofuata hatujaona mpango wowote ambao unaelekea pale, kwa maana kwamba kuna fedha yoyote ambayo inakwenda kutimiza huu mpango. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nisisitize kwenye suala la upatikanaji wa mabwawa katika mkoa huu. Mkoa wa Simiyu una maeneo makubwa sana ya kilimo cha umwagiliaji. Kwa mfano, kama maeneo ya Matongo, Mwamtani, Meatu, Malampaka, Malampaka ni walimaji wazuri wa mipunga na mazao mengine. Kwa hiyo, ni vyema Serikali hii ikajikita sana kututengenezea mabwawa ili Wasukuma waendelee kulima kilimo cha umwagiliaji. Tumechoka kuletewa chakula cha msaada kutoka Serikalini ambacho tukiletewa tunapewa kilo tatu.
Ndugu zangu Wasukuma tunazaa mpaka Mungu aseme wametosha, ukiniletea kilo tatu, kwa kweli hiyo mimi naona siyo sahihi. Kwa hiyo, niombe sana kwamba ifike mwisho, mkoa wetu usiwe tegemezi kwenye chakula cha msaada na badala yake tujisimamie na tuweze kuendana na kasi hii ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, masikitiko yangu makubwa ni kwamba, ziwa linatuzunguka, lakini hatupati maji safi na salama. Kwa mfano, Mikoa kama ya Mara, Mji wa Tarime hauna maji, kuna bwawa moja tu la wakoloni ambalo hata usafi halifanyiwi la miaka nenda rudi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana Mkoa wa Mara, Mkoa wa Simiyu, Mikoa hiyo ipate maji safi na salama ili tuendane na kasi ya Serikali hii ya Awamu ya Tano. Kwa hiyo, niombe sana na Wabunge wenzangu tunaotoka Mkoa wa Simiyu tusichoke kupiga kelele kuhusu mkoa wetu angalau tuone ni jinsi gani Serikali yetu itaweza kutusaidia ili tupate angalau hata robo tatu ya mafanikio ambayo tunayatarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabisa Mheshimiwa Waziri, Wabunge waliokuja Awamu hii ya Tano tusipopeleka maji Mkoa wa Simiyu nawahakikishia 2020, hakuna Mbunge atakayekuja hapa, hakika wananchi wamechoka kunywa maji ya chumvi. Sasa hivi tumeanza kupata matusi kutoka kwa Wabunge wenzetu kwamba tumeoza meno, si kwamba tumeoza meno kwa sababu hatupigi miswaki, hapana tumeoza meno kwa sababu tunatumia maji ambayo yana chumvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niombe sana Mheshimiwa Waziri, badala ya kuendelea kupata matusi haya basi ifike mahaliā€¦