Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja hii ambayo ipo mbele yetu; hoja ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Pia niungane na wenzangu kwa kumpongeza Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mheshimiwa Engineer Lwenge na Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kamwelwe. Pia nawapongeza Watendaji; Engineer Mbogo na Naibu Katibu Mkuu, Engineer Kalobelwe. Sina mashaka na watu hawa, ni watendaji wazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanzia tu, katika Jimbo letu la Nanyamba tunamshukuru sana Naibu Waziri wa Maji kwa sababu ndiyo Naibu Waziri wa kwanza katika Awamu hii ya Tano kufika katika Halmashauri yetu mpya ya Nanyamba. Alifanya ziara, alitembelea lakini sina wasiwasi na Waziri mwenyewe kwa sababu na-declare interest, kabla sijaingia kwenye siasa nilikuwa Mkurugenzi huko nyuma, alishafika mpaka Newala na nikampeleka katika mradi wa maji wa Makonde. Kwa hiyo, hata hiki ninachokiongea, anafahamu maeneo hayo na miradi hiyo ninayoizungumzia hapa anaifahamu kwa undani wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia hoja yangu kuhusu suala la takwimu. Naomba sana niishauri Wizara kwamba tumefikia asilimia 72, lakini tuna changamoto kwamba hii asilimia 72 ni asilimia ya jumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto sasa ya kwenda case by case kwenye kata, kwenye wilaya na kwenye mikoa. Kuna tofauti kubwa sana! Katika Jimbo langu, upatikanaji wa maji vijijini sasa hivi ni asilimia 40. Jirani yangu Tandahimba kwa Mheshimiwa Katani ni asilimia 45; jirani yangu Mheshimiwa Mkuchika pale amesema pale vile vile ni asilimia 47. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wakati National average ni hiyo 72, kuna maeneo wako chini sana. Kwa hiyo, hata tunapo-design miradi yetu, tuangalie sasa kwamba hali ya upatikanaji wa maji katika kila kata, wilaya na mkoa ikoje, ndiyo hapo tutatenda haki na kutengeneza miradi ambayo itajibu kero za wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwakumbushe vile vile kwamba kwa kweli hakuna maendeleo bila maji. Pili, maji ni siasa kama walivyosema watu wengi. Asilimia kubwa ya akinamama wanatumia muda wao mwingi sana badala ya kushughulika na shughuli za maendeleo, wapo wanahangaika na maji. Kwa hiyo, tukipeleka maji vijijini, tutaokoa kundi kubwa la akinamama ambao wanahangaika na maji na watafanya shughuli za maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi magonjwa mengi ambayo yanaathiri watu wetu ni kwa sababu ya kutokupatikana kwa maji safi na salama. Tukipata maji safi na salama, basi tutakuwa tumezuia hizo gharama ambazo tunazitumia kwa ajili ya kutibu magonjwa hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nijielekeze kwenye mradi wa maji wa Makonde. Sitarudia yale ambayo yamesemwa na Mheshimiwa Mkuchika, lakini nisisitize tu kwamba, kwa Wizara sasa mchukue hatua, huu mradi ni mkubwa, wa siku nyingi na umechakaa. Pale Mitema ukifika kuna kazi inahitajika kufanywa. Hebu tuwekeze vya kutosha ili tumalize suala la maji Newala, Tandahimba na Nanyamba. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotakiwa kufanywa sasa hivi ni ukarabati mkubwa ambao unaendelea pale Mitema. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa jitihada zake kwamba kuna kazi inaendelea kule sasa hivi, lakini kuna kazi imebaki, lazima tubadilishe mabomba, umbali wa kilometa nane kutoka pale Mitema kwenda Nanda; na tukifanya hivyo tutakuwa tumeboresha upatikanaji wa maji Tandahimba.
Pili, wakati Mheshimiwa Naibu Waziri alipotembelea, tulikabidhi andiko letu ambalo silioni kwenye vitabu vyake hapa, lakini naamini kwamba ahadi ya Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na ahadi ya Serikali, bado naendelea kuamini kwamba ataendelea kuyafanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mradi pale tulipendekeza na andiko limeshakabidhiwa kwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa kutoa maji Kijiji cha Lyenje na kupeleka Nanyamba. Mradi huu utanufaisha kata tisa, vijiji 43 na wananchi takriban 24,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hawa ni watu wetu, wanahitaji maji na wana shida kubwa sana ya maji. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kufanya sum up atuambie kwamba andiko lile sasa wana-accommodate vipi kwenye ukarabati mkubwa wa mradi wa Makonde ambao napongeza jitihada za Wizara yake kwa sababu bado anaendelea kufanya mazungumzo na Serikali ya India ili tupate fedha kwa ajili ya mradi huu mkubwa. Kwa hiyo, naomba na hili andiko letu sasa la kuchepusha maji Lyenje na kwenda Nanyamba, basi lifanyiwe kazi ili fedha zikipatikana miradi hiyo yote iweze kutekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie vile vile kuhusu mradi wa kutoa maji Mto Ruvuma kupeleka Manispaa ya Mtwara Mikindani. Naipongeza Serikali yangu ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi kwa jitihada ambazo imezifanya, kwa sababu mradi huu ukitekelezwa utakuwa umemaliza tatizo la maji Manispaa ya Mtwara. Kwa sababu kama iliyoelezwa kwenye kitabu, upatikaji wa maji sasa hivi ni lita milioni tisa lakini mradi huu ukikamilika, tutakuwa na uhakika wa lita milioni 120.
Kwa hiyo, mahitaji ya maji Dangote na viwanda vingine vyote ambavyo vitafunguliwa Manispaa ya Mtwara hatutakuwa na maji. Huku ndiko kutengeneza mazingira wezeshi kwa wawekezaji wetu. Kwa hiyo tukikamilisha mradi huu basi tutakuwa tumetengeneza hata mazingira mazuri ya uwekezaji katika Manispaa yetu ya Mtwara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina ushauri. Maji haya tunayatoa Mto Ruvuma kwenye Kijiji cha Maembe Chini ambako ni Jimbo langu. Mheshimiwa Waziri amesema vijiji 26 vitafaidika, lakini naomba tuongeze idadi ya vijiji. Tunaweza tukaongeza idadi ya vijiji kiasi kwamba Kata ya Kiromba, Kitaya, Mbembaleo, Chawi na Kiyanga wakafaidika na mradi huu; na hiki kinawezekana na nilijadiliana muda fulani na Naibu Waziri akasema watalifanyia kazi. Naomba sana walifanyie kazi ili wananchi hawa wafaidike na mradi huu mkubwa.
tukianzisha mamlaka bila kuwa na maji ya kutosha…
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.