Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema aliyeniwezesha na kunipa afya njema na uzima wa kuniwezesha leo hii nichangie kwa maandishi katika Wizara ya Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya utalii ni moja ya sekta muhimu sana na kwa hakika ni sekta ambayo ikipewa msukumo wa nafasi ya kipekee, italiongezea Taifa letu fedha nyingi. Mbuga zetu za hifadhi ambazo ni vivutio vya watalii zinahitaji kuwekewa mazingira mazuri ambayo yatawavutia watalii, naomba nitoe mifano miwili ya mbuga za Ruaha na Saadani, barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Mbuga ya Ruaha siyo ya kiwango cha lami, na vivyo hivyo barabara itokayo Tanga kwenda Pangani hadi Saadani ni mbuga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali hii naiomba Serikali iangalie kwa jicho la kipekee kama biashara nyingine zilivyo na ushindani, Serikali iongeze kasi katika kuutangaza utalii wetu. Bodi ya Utalii ishirikiane na wadau mbalimbali wa sekta binafsi kufanya jitihada hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, kwa hotuba nzuri yenye kuonesha mwelekeo, nampongeza pia Naibu Waziri pamoja na watendaji wote wa Wizara na nawatakia kila la kheri, wasonge mbele na kasi hii ya hapa kazi tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja mia kwa mia.