Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naunga mkono hoja hii na kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji mzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepitia hoja mengi yana dira nzuri kwa maana ya msimamizi wa sheria. Tatizo langu ni namna watendaji na hasa wanaosimamia hifadhi ya maeneo wanapochukua sheria mikononi na kupigana, kushambulia wananchi. Wanahisiwa kuingia ndani ya maeneo hayo, Jimbo langu lina mgogoro katika maeneo mawili yaani Hifadhi ya Kipengere na Mpanga Game Reserve, vijiji vinavyopakana na maeneo haya vya Moronga, Kipengere, Masage, Wangana, Ikunga na Imalilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawana amani na maeneo yao, pamoja na kuwa vijiji hivi vimeidhinishwa na vina ramani ya mpaka jinsi wanavyonyanyaswa na Kipengere Forest Reserve.
Aidha, vijiji vya Malagali, Mpaga, Ludunga, Mambegu, Hamjarami, Igando, Iyayi, Mayole na Mpanga Game Reserve wananchi walihamishwa wakalipwa fidia kidogo na kuhamishwa wengi hata fidia hawakulipwa. Naomba sana viongozi walioko hifadhi hii ya Mpaga waondolewe kwani wameshindwa kabisa kufanya kazi na viongozi wa Wilaya, Serikali na Vijiji na Mbunge wa Wilaya ya Wapingale kwa namna wanavyochukua sheria mkononi kwa kuwapiga wananchi, kufyeka mazao na kuwanyang‟anya mifugo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu hawa wanachukua rushwa, tumewakemea na Waziri nilikueleza, lakini mpaka leo hakuna hatua iliyochukuliwa. Naomba na wakati hilo halijafanyika wape maelezo viongozi wa hifadhi hizi, waache mara moja kuwashambulia raia kwenye nchi yao ili tulishughulikie tatizo la mpaka. Ili kuondoa migogoro hii pamoja na sheria lazima ziwe na manufaa kwa binadamu na uhifadhi ili sheria iwe endelevu. Sheria ilitungwa na Mipaka iliwekwa miaka mingi baada ya uhuru, wakati idadi ya watu ilikuwa ndogo tofauti na sasa, lazima wananchi wetu waongezewe eneo na hasa haya maeneo ya akiba ambayo hata wanyama hawapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 51 nimesoma kuwa Mfuko wa Kuhifadhi Wanyamapori umesaidia miradi ya kijamii kwenye Wilaya ya Wanging‟ombe kwa kujenga Ofisi ya Kata ya Wanging‟ombe, kuchimba kisima Mayale, na kununua vitanda 91 vya shule ya bweni sekondari Ilembula. Kwanza nashukuru kama kweli limefanyika, naomba kujua kiasi cha fedha zilizopelekwa au thamani ya vifaa kwa kila mradi.
Pili, utekelezaji wa msaada huu hufanyika vipi kwani mimi kama Mbunge ndiyo kwanza napata taarifa hii kwenye kitabu cha hotuba, sijawahi kushirikishwa wala kwenye Halmashauri ya Wanging‟ombe hatujawahi kushirikishwa. Sasa hii kama fedha ya umma kwa nini ifanywe siri kwa ajenda gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipate maelezo ya kina.