Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naanza kutoa mchango wangu kwa kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuwa Mbunge wa Bunge hili. Pili nawashukuru wapiga kura wangu kwa kunichagua kwa kura nyingi kuwa Mbunge wao, natambua imani kubwa waliyonayo kwangu na nawaahidi nitawatumikia kwa nguvu zangu zote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Rais wetu Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kuonesha imani na uwezo mkubwa wa kuendesha nchi yetu, Mungu ampe umri na afya njema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne napenda kumpongeza Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa pamoja na Baraza lake la Mawaziri kwa kuonesha uwezo mkubwa wa kuongoza Wizara zao. Katika kuchangia hotuba ya Waziri napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta ndogo ya ufugaji, kumekuwa na migogoro isiyomalizika kati ya sekta ya ufugaji na wakulima. Hili ni tatizo ambalo Wizara hii inapaswa kulishughulikia kwa namna ya pekee. Naomba Wizara ianzishe idara maalum ndani ya Wizara hii ya kushughulikia migogoro hii ili kuondosha kabisa tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta ndogo ya utalii, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 15 imeeleza hali ya sekta hii inavyochangia upatikanaji wa fedha. Takwimu zinaonesha kwenye ukurasa huu ni ndogo, hazilingani na namna uingiaji wa watalii katika nchi yetu. Watalii wanaoingia ni wengi sana hivyo nashauri Wizara ichukue mikakati zaidi ya kuziba mianya ya upotevu wa fedha za watalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori. Nachukua fursa hii kuipongeza Wizara kwa kuanzisha mamlaka hii ni jambo zuri katika kusimamia na kuwalinda wanyama pori wetu. Nashauri Wizara iharakishe kupeleka mamlaka hii katika Wilaya zote za nchi ili huduma hii ipatikane nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.