Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Anna Joram Gidarya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya ardhi kati ya wakulima, wafugafji na hifadhi ya Tarangire, kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya wananchi na hifadhi ya Tarangire, Mkoani Manyara jambo ambalo limewagharimu wananchi na hata kukosa makazi ya kuishi baada ya kutolewa katika maeneo yao kwa madai kuwa wamevamia Hifadhi ya Tarangire.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu mwaka 2007 wananchi wa vijiji vya Ayamango, Gedamara na Gijedabung‟ hawana makazi maalum wala maeneo ya kulima kujipatia kipato na hata chakula kwa ajili ya matumizi ya kawaida pamoja na kuwa Serikali inasema kuwa wamepata eneo mbadala ya kuwahamishia wananchi hao ambao ni shamba la mmiliki Ufyomi Gallapo Estate. Shamba hilo ni dogo sana, halitoshi kukidhi mahitaji ya wananchi hao kulima na maeneo ya kujenga nyumba bora.
Pamoja na juhudi za Serikali kuwahaminisha wananchi hao hakuna makubaliano kati ya Serikali na mmiliki huyo na wala hakuna mkutano wa hadhara uliokaa kwa vijiji vyote hivyo kuwaeleza hatua zilizochukuliwa na Serikali kumfutia mmiliki wa Ufyumi Gallapo Estate. Ni lini Serikali itamaliza mgogoro huu kwa kuwakabidhi wananchi hao eneo mbadala ili waendelee na maisha ya kila siku ya kujitafutia riziki zao za kila siku katika shughuli za kilimo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ya wanyama Burunge, mgogoro wa vijiji vya Maweni Magara, Manyara Kisangaji na Kazaroho ni wa muda mrefu sana kati ya Juhibu na wafugaji pamoja na wakulima. Jumuiya ya Juhibu inaundwa na vijiji kumi ambayo ni Minjingu, Mdori, Kisangaji, Kazaroho, Maweni, Magara, Manyara, Ngoley, Mwanda na Nkaiti. Huo ndiyo muunganiko wa vijiji kumi vilivyounda Jumuiya ya Hifadhi ya wanyama Burunge kwa makubaliano ya kutenga matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo ya wakulima, wafugaji na uhifadhi ambayo ndiyo Juhibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mapato yatokanayo na Juhibu hugawanywa kwa vijiji wanachama kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya vijiji husika. Lakini cha kushangaza leo hii wakulima na wafugaji wanaondolewa katika maeneo yale kwa nguvu ya dola jambo ambalo ni la kikatili na unyanyasaji hata kufikia wananchi kuchomewa nyumba na mifugo na askari wa Juhibu na kuwataka wananchi hao kuhama ifikapo tarehe 1/6/2016 kwenda kwenye eneo mbadala la Mfula Ng‟ombe ambao ni eneo la madimbwi ya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba kuhusu wananchi wa vijiji vya Ayamango, Gidamara na Gijedabung‟ Serikali ifanye jitihada za haraka sana kuwapatia wananchi wale eneo mbadala lililotengwa hata kama ni vipande ili waendelee kuiamini Serikali yao na kuipa matumaini mapya ya kujikwamua kiuchumi na kimaisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vijiji vinavyounga Juhibu naishauri Serikali eneo lililotengwa kwa ajili ya wananchi wale kuhamia halifai kwani eneo lile la Mfula Ng‟ombe lina historia ya kuwa na kichocho kutokana na madimbwi ya maji yaliyozunguka eneo lile. Hivyo halifai kwa makazi ya binadamu kuishi eneo lile.