Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa ya kuchangia kwa maandishi. Napenda kuipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa hotuba nzuri, lakini pamoja na yote, napenda kuwataarifu Waziri na Naibu wake kwamba kwa haraka haraka inaonekana watendaji wa Wizara hii wanafanya kazi kwa mazoea na ni wakati sasa wa watendaji hawa kusimamia Katiba ya nchi pamoja na Sera Taifa zinazoigusa Wizara hii ikiwemo Sera ya Taifa ya Mifugo ya mwaka 2006.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wajibu wa Wizara hii kuhakikisha kwamba utalii wa nchi yetu unaimarika kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwemo ile ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyomo ndani ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha kuona nchi nyingine zikijitangaza kuwa na baadhi ya vivutio vilivyopo ndani ya nchi yetu kama come to Kenya and see Mount Kilimanjaro. Hili ni suala la kusikitisha sana pale nchi yetu inaposhindwa kukemea masuala haya kupitia Serikali yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashangaa kwa umri wangu sikuwahi kusikia kitu chochote kuhusu mjusi wa aina ya dinosaur aliyewahi kupatikana hapa nchini Tanzania Mkoa wa Lindi na kupelekwa Ujerumani. Nimekuwa na maswali mengi juu ya hili. Nimekuwa nikijiuliza ni kiasi gani cha fedha Ujerumani inaingiza kupitia huyu mjusi? Katika hizo fedha ni kiasi gani kinaletwa Tanzania na ni kiasi gani kinapelekwa Lindi kwa ajili ya maendeleo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha sana kuona hata mashuleni hili halitajwi popote na kibaya zaidi hata huko Ujerumani hatuna uhakika kama hawa wanataja mnyama huyo katokea Tanzania na kibaya zaidi historia ya mjusi huyu haijulikani na ipo mbioni kupotea kabisa tukizingatia uwepo wa kizazi hiki na kijacho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Wizara husika kutueleza ni shilingi ngapi tunaingiza kama nchi kutokana na mjusi huyu na ni jinsi gani tunafaidi kwa yeye kuwepo huko Ujerumani? Ninaisihi Serikali kumrudisha mjusi huyu nchini ili tuongeze kipato cha Serikali kupitia utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuiomba Wizara hii kuwapeleka Madiwani wa sehemu husika alipopatikana mjusi huyu na baadhi ya Wabunge wakiwemo wanaotoka Lindi kwenda kumuona mjusi huyu ili waje watuhakikishie uhai wake, lakini kikubwa zaidi tupate taarifa ya kujiridhisha juu ya kipato anachoingiza nchini humo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango huu, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante.