Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. QULWI W. QAMBALO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imejaaliwa sana kwa kuwa na vivutio vya utalii hadi kushika nafasi ya pili duniani. Hii ni zawadi na heshima kubwa aliyotupa Mwenyezi Mungu. Si watu wote nchini wanafurahi na kuwepo hifadhi za wanyama katika maeneo yao kutokana na manyanyaso na uonevu wanaofanyiwa na hifadhi hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) haitendei haki wananchi wa vijiji vinavyozunguka. Mipaka ya Hifadhi ya Ngorongoro iliwekwa tangu mkoloni na inafahamika na beacons zipo katika mazingira ya ajabu sana. Mwaka 2002/2003 NCAA walifanya uhakiki wa mipaka yao na hapo ndipo walipopora maeneo ya wananchi ya malisho ya mifugo yao katika vijiji vya Endamaghang na Losetete. Tangu muda huo migogoro imeshamiri. Ikumbukwe wakazi wa kijiji cha Losetete walihamishiwa Lositete miaka ya 1950. Kuchua maeneo yao waliyopewa ni unyanyaswaji wa hali ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Wizara ya Ardhi imefanya uhakiki wa mipaka ya NCAA. NCAA ndiyo waliolipa fedha ya zoezi hilo na nitahadharishe Wizara kuwa isije ikawa uhakiki unaofanywa sasa ni kutaka kuhalalisha haramu iliyofanyika mwaka 2002/2003 walipohakiki. Nawataka NCAA wahakiki mipaka yao ya awali na siyo mipaka ya mwaka 2002/2003 waliyojiwekea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni uharibifu unaofanywa na wanyama kutoka Ngorongoro (ndovu na nyati) kwenye mashamba ya wanavijiji katika vijiji vya Lositete, Kambisimba, Kambi ya Nyoka, Oldeani na Makulivomba. Wananchi wanajitahidi kulima lakini wanyama wanawatia umaskini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la ajabu ndovu wanatoka crater hadi barabara ya lami iendayo Ngorongoro, askari wa doria hawatoshi na pia hawajawezeshwa. Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha, aliambie Bunge hili Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa uharibifu wa mashamba ya wananchi unaofanywa na wanyama unadhibitiwa?