Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza hotuba ya Wizara ya Maliasili na Utalii na ninaunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vya utalii vipo Kaskazini mwa nchi yetu. Nashauri Serikali ianzishe kituo kingine cha utalii Kusini mwa nchi yetu. Utalii siyo kuona wanyama pori tu, hata bahari yetu ya Lindi na ngoma za utamaduni. Ujenzi pia wa hoteli kubwa upande wa Kusini zinaweza kufanya watu wengi kutembelea Kusini na kuja kuona mambo mbalimbali na kuliongezea Taifa letu uchumi na mapato. Pia tunayo Selous ya Liwale. Naomba iboreshwe ili watu wengi waje Liwale kwa ajili ya kuona wanyama na uwindaji halali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua atakapokuja kufanya hitimisho, Mheshimiwa Waziri atueleze tunaye mjusi yule mkubwa aliyepo Ujerumani (dinosaur) anayeingiza mapato kule Ujerumani. Mjusi huyu aliyetoka mkoani Lindi, kijiji cha Mipingo. Sisi Tanzania tunapata nini katika mapato yale yanayoingia Ujerumani kupitia mjusi huyu? Kijiji hiki cha Mipingo kinafaidikaje na mjusi huyu? Napenda kupata taarifa ya maswali haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana.