Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, naomba kumpongeza sana Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe na Naibu Waziri Mheshimiwa Engineer Ramo Makani, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Wakurugenzi na watendaji wote wa Wizara, Wakuu wa Mashirika na Taasisi zote zinazohusiana na Wizara hii. Baada ya pongezi hizo, naomba sasa kueleza yangu machache.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ni kati ya hifadhi chache zinazoingizia nchi yetu Tanzania pato kubwa sana la fedha za kigeni. Mlima huu unayo theluji kileleni ambayo inapungua siku hadi siku. Haya ni matokeo ya tabia nchi, lakini ukame unachangia sana. Hakuna mashaka kabisa kuwa ukame unaweza kupunguzwa kwa kuotesha miti maeneo yanayozunguka mlima. Jambo hili linawezekana kabisa endapo wanakijiji watapatiwa miche.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali ni lini Serikali itaagiza miche kwa wanavijiji hawa ili waoteshe kwa nguvu zote? Nitapenda kupata majibu wakati Mheshimiwa Waziri atakapokuwa anahitimisha hoja yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mgao wa asilimia 25 wa mapato ya mlima kwa Halmashauri zinazozunguka mlima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na ninaunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.