Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nachukua fursa hii kumpongeza sana Waziri wa Maliasili Utalii Profesa Maghembe, Naibu wake Engineer Ramo Makani kwa kazi nzuri sana wanayofanya kwa Wizara hii, kumbukeni methali ile isemayo mti wenye matunda hauishi kutupiwa mawe. Hata hivyo mmeweza na tunawatakia kazi njema na ya ufanisi kwa maendeleo ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninazo hoja zangu kadhaa ambazo naomba mnapo-wind up mnipatie majibu.
(i) Burunge Game Control Area iliyoko Makuyuni na Babati Vijijini ni eneo kubwa sana igawanywe ili ibakie sehemu ndogo tu na nyingine irudishiwe wananchi na hivyo sheria iliyoko ibadilishwe kuruhusu mapendekezo hayo.
(ii) WMA iliyoko eneo la Vilima Vitatu Babati ni mateso makubwa kwa wafugaji walioko eneo lile, kiasilia eneo hilo lilikuwa la wafugaji na hata baada ya kushtakiana na WMA wafugaji walishindwa kesi. Hadi leo wananchi hao hawajapewa haki yao, naiomba Wizara ilishughulikie suala hili kuwapa wananchi wa Vilima Vitatu utulivu wa maisha na usalama wa maisha yao na mifugo yao. Naomba kauli ya Wizara.;
(iii) Vijiji 16 vinavyozunguka hifadhi ya Tarangire na Magugu walipoondolewa waliambiwa watapewa kifuta jasho hadi leo kati ya fedha walizoahidiwa Tanzania zaidi ya shilingi milioni 100 wamepewa shilingi milioni 12 tu. Huu ni unyanyasaji wa wananchi. Naomba msaada wako Professa na naomba kauli ya Serikali.
(iv) Wananchi wanaozunguka Hifadhi za Ayamango, Gedamar na Giijedabonga – Babati wako pale tangu Operesheni Vijiji, leo na kwa muda mrefu ndani ya hifadhi isitoshe wengi wao hawajaonyeshwa maeneo ya kuhamia kila mara ni mapambano na askari na wanyamapori. Mheshimiwa Profesa na Engineer (Wizara) naomba sana mtoe suluhu ya migogoro hii, fidia wanayopewa haijengi hata choo.
(v) Wakati wa Operesheni Tokomeza aliuwawa mwanamke kwa maelezo yaliyotolewa hata hapa Bungeni na kwenye vyombo vya habari, Serikali iliunda Tume ya Kijaji na hadi leo hii hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Serikali. Mheshimiwa Jitu amewaandikia barua bila majibu yoyote, naiomba Wizara itoe kauli juu ya jambo hili linalosubiriwa na wananchi wa Babati na Mkoa wa Manyara.
(vi) Halmashauri ya Wilaya zinazopaswa kupata asilimia 0.3 ya service levy za hoteli za kitalii zinazopaswa kulipa Halmashauri lakini hoteli zimegoma kulipa kiasi hicho mpaka Mahakama ya Rufaa, lakini Wizara imekaa kimya. Tunaomba ufumbuzi wa malipo haya ya asilimia 0.3 service levy kwa Halmashauri husika hapa nchini ni imani yangu Mheshimiwa Waziri utatolea kauli.
(vii) Tanzania Forest Service wanakusanya ushuru mkubwa kutokana na mkaa wa magogo. Naiomba na naishauri Serikali kuwa taasisi hii irudishe kiasi fulani cha mauzo haya ili kuendeleza upandaji wa miti itafika mahali misitu itaisha.