Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, lakini naomba niwashauri katika maeneo mbalimbali ili kuboresha na kustawisha Wizara ambayo ni nyeti katika kuongeza Pato la Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri sana inayofanywa na Mheshimiwa Waziri na viongozi wenzako nashauri kuchukua mapendekezo mazuri yaliyotolewa na Kamati pamoja na ushauri mzuri unaotolewa na Waheshimiwa Wabunge kwa mustakabali wa nchi.
Pia katika kutatua migogoro ndani ya hifadhi Waziri kupitia wataalam wake watatue migogoro kwa kuzingatia hekima, busara na taratibu za kisheria zilizopo, wasitumie mabavu, tunajua sheria zipo lakini tatizo ni ushirikishwaji hafifu au elimu duni ya uhifadhi ikichangiwa na rushwa.
Mheshimiwa Waziri, Shirika la Hifadhi za Taifa linalosimamia Hifadhi za Taifa 16 hadi leo halina bodi kwa mujibu wa Sheria Sura 282 ya mwaka 2002 na kama ilivyorejewa kwa Sheria ya Hifadhi za Taifa ya mwaka1959 Sehemu ya II inayoanzisha Hifadhi ya Taifa na Bodi ya Wadhamini. Nashauri kufuatana na uzito na umuhimu wa taasisi hii Waziri umwombe Mheshimiwa Rais ateue Mwenyekiti wa Bodi na wewe uteue Wajumbe wa Bodi haingii akilini taasisi kubwa kama hii kukaa miaka zaidi ya minne bila Bodi ya Wadhamini.
Naomba niulize, TANAPA kutokuwa na bodi ni nani anaamua maamuzi ambayo uamuzi wake unatakiwa uamuliwe na bodi. Mheshimiwa Waziri Chuo cha Mweka nikiwa Mjumbe wa Bodi kwa wakati huo Rais wa Awamu ya Nne alitamka kwa kumwambia Waziri wa wakati huo Mheshimiwa Mwangunga kuwa chuo hicho kiwe chuo cha mfano (center of excellence) lakini hayo hatuyaoni, kumbuka chuo hicho ndicho kiwanda cha kuzalisha wataalamu katika tasnia ya wanyamapori hasa katika hifadhi zetu zote nchini. Nashauri chuo hicho pamoja na kile cha Pasiansi visimamiwe vizuri ili kutoa wataalam na askari wanaoweza kwenda kusimamia vizuri maeneo ya uhifadhi.
Nimalize kwa kuwaomba viongozi wote walio chini ya Wizara hii kumsaidia Waziri ili yaliyoainishwa ndani ya kitabu hiki yaweze kutekelezwa. Lakini kwa pekee nimpongeze CEO wa TANAPA kwa kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa pamoja na kutokuwa na Bodi ya Wadhamini.
Mheshimiwa Waziri moja ya changamoto kubwa ni kutopata takwimu sahihi za watalii hasa katika eneo la Selous, Serikali iangaie njia nzuri zaidi hasa kwa hawa wenye hoteli ziwe na takwimu sahihi ili kudhibiti mapato ya Serikali lakini kuwe na motisha kwa wafanyakazi na Selous iimarishe usimamizi kwa kila hoteli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika pori la akiba la Selous lina jumla ya kambi za kuweka wageni (camp sites) nane na zisizopewa wawekezaji hadi leo hawajaendeleza, nashauri wanyang‟anywe ili wapewe wengine na kuendelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuondokana na uvamizi wa maeneo yaliyohifadhiwa kwa ajili ya makazi, kilimo, ufugaji na matumizi endelevu nashauri kuainisha na kuhakiki mipaka ya mapori ya akiba kwa mujibu wa GN kupitia Wizara ya Ardhi, kutoa elimu ya uhifadhi na kufanya tathmini ya mapori tengefu. Pia nashauri kuzishirikisha Wizara na taasisi zingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Utalii (TTB) na TANAPA kwa pamoja na NCCA hawajaonyesha jitihada za kutangaza utalii nje na ndani ya nchi. Je, ni kwa nini taasisi hizo ikiwemo Bodi ya Utalii hawatilii mkazo suala zima la kutangaza na kuondoa vikwazo vinavyokwamisha watalii hasa wa Marekani na Wafaransa ili ile idadi ya watalii iongezeke na nchi ifaidike na utalii kwa kuongeza mapato zaidi.