Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kuendelea kunipa uzima na afya njema, na leo naomba nichangie hoja hii ya maliasili na utalii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Mikindani upo Manispaa ya Mtwara Mikindani ambalo ni jimbo langu. Mji huu ni mji wa asili ambao una magofu na vivutio vingi vya utalii ikiwemo Old Boma ambayo ilijengwa na Mjerumani kama ngome yake kuu ya ulinzi karne ya 19. Cha ajabu, mji huu umesahaulika, umeachwa na jambo la ajabu kabisa yanatangazwa maeneo ambayo hayana vivutio kama Mikindani. Namuomba Waziri aje na majibu juu ya kuutangaza mji huu kuwa ni mji wa kitalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mtwara kuna fukwe nyingi nzuri sana ambazo kama Serikali ikitangaza watalii wengi wanaweza kuja Mtwara na hatimaye Taifa hili kupata kipato kikubwa kupitia sekta hii. Nimeuliza swali la utalii Mtwara tangu kipindi cha Kikao cha Kwanza katika Bunge lako hili mpaka leo sijapata majibu. Namtaka Waziri akija anieleze, yupo tayari hivi sasa kutangaza fukwe za Mtwara sambamba na kuzitambua katika Wizara yake kuwa kitovu kikuu cha utalii?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Msimbati, Mnazibay kuna fukwe ambayo haipo duniani na kuna maua ambayo hayapo na hayaoti popote duniani isipokuwa Mnazibay tu. Nimuombe Waziri aje Mtwara nifuatane naye kama Mbunge, na asije kimya kimya ili nimuoneshe vivutio hivi vya utalii Mtwara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Lindi eneo la Mipingo, Kata ya Nangaru alichukuliwa mjusi na Wajerumani ambaye mabaki yake yapo Ujerumani. Tangu mwaka 1907 mpaka leo Wajerumani wanapata pesa nyingi kupitia mjusi huyu
mkubwa kuliko mijusi yote duniani. Serikali hii ya CCM ni lini itaenda kumrudisha mjusi huyu na kumleta Tanzania ili tunufaike na pesa za utalii?