Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja. Aidha, niwapongeze sana Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa wanayoifanya pamoja na kuwa na changamoto nyingi, Mungu mweza wa yote awatie nguvu, mtende kazi bila kuchoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ni tamaduni za makabila; niwaombe katika suala la utalii muangalie pia historia na tamaduni za makabila mbalimbali kwani chaweza kuwa kivutio kikubwa cha utalii, kupata historia na utamaduni wa makabila husika. Mfano Kituo cha Bujora na Kayenze Mkoa wa Mwanza, kwa Wanyamwezi Tabora (Mwinamila), tamaduni na historia za Mkoa wa Kagera, Mkoa wa Katavi, Mkoa wa Iringa na Mkoa wa Ruvuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Makumbusho ya Mkwawa - Iringa, kuna mengi ya kuvutia watalii, lakini pamesahaulika sana. Historia ya Mkwawa hakuna asiyeifahamu lakini kituo chake kimesahulika sana na pamechakaa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu fidia kwa waathirka wa kung‟atwa na fisi; Jimboni kwangu katika Kata ya Sangabuye na Bugogwa zaidi ya watu nane waling‟atwa na fisi na wawili hali zao zilikuwa mbaya sana. Halmashauri italeta madai ya wananchi wakidai fidia kwa madhara waliyoyapata. Vilevile kwa habari nilizopewa, ninaomba walete ushahidi wao baadhi yao walipwe fidia siku za nyuma. Ninaomba mara watakapoleta madai yao yashughulikiwe mapema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wafugaji na wakulima; ni vyema kama ambavyo imesemwa mara nyingi na Wizara yetu imelizungumzia, tupange kukutana na Wizara zinazohusika ili tumalize kero hii, watu wawe wafugaji wasiosumbuliwa. Iwapo kuna haja ya kumega maeneo ambayo yamevamiwa na makazi ya watu, tupime uzito ili kuondoa kero na kelele za mara kwa mara. Lengo la Serikali ni kuondoa kero, lakini kuwafanya wananchi waheshimiu sheria za nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la elimu liwe endelevu ili watambue mipaka yao, zaidi sana wawe sehemu ya kulinda mazingira na hifadhi zetu.