Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia katika Wizara hii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na changamoto ya uchomaji wa misitu hovyo hasa kipindi cha miezi ya saba hadi kumi na moja. Tatizo hilo la uchomaji limekuwa kubwa sana na la kawaida katika Mkoa wa Njombe, katika maeneo ya Kifanya na maeneo mengine. Napenda kuishauri Serikali kusimamia sheria lakini pia wachukue hatua kali dhidi ya wananchi watakaobainika wanachoma moto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kumekuwa na changamoto ya TANAPA kufyeka mahindi, ndizi, miwa katika kijiji cha Luduga, Wilaya ya Wanging‟ombe. Nashauri Serikali itoe elimu kwa wananchi wa maeneo hayo kuhusu maeneo ya hifadhi na kuweka mipaka kati ya hifadhi na maeneo ya kulima wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wafanyakazi wa hifadhi wasinyanyase wananchi kwa kuwapiga na kuwapeleka kwenye vituo vya polisi. Wawe na
uzalendo wa kujadiliana badala ya kutumia nguvu kwa kuwafyekea mazao yao na huo sio ubinadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha, ahsante.