Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua nafasi hii kwa kifupi nichangie hotuba ya Waziri wa Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukataji miti hovyo ni chanzo kikubwa sana kinachochangia mabadiliko ya hali ya hewa ikiwa ni pamoja na nchi yetu kuelekea kuwa jangwa. Uchomaji wa mikaa hovyo nao pia unachangia sana mabadiliko ya hali ya hewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na uharibifu mkubwa sana juu wa vyanzo vya maji kutokana na matumzi mabaya ya ardhi. Kwa nini:-
(a) Halmashauri zetu zinaruhusu wananchi kujenga ndani ya vyanzo vya maji, sheria ifuate mkondo wake.
(b) Uchimbaji wa mchanga na kokoto navyo vinachangia uharibifu wa vyanzo vya maji, sheria ifuate mkondo wake.
(c) Shughuli za kilimo ndani ya vyanzo vya maji nalo ni tatizo kubwa, sheria ifuate mkondo wake.
(d) Shughuli za ufugaji ndani ya vyanzo vya maji zidhibitiwe ili vyanzo vyetu visiendelee kuharibiwa.
(e) Tusiruhusu nchi jirani kuingiza mifugo katika nchi yetu, ni hatari sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono michango ya TANAPA kwa jamii na nawapongeza kwa dhati na niombe taasisi au mawakala wengine wa Serikali kama TANAPA watoe mchango kwa jamii kama TANAPA wanavyofanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mabadiliko ya hali ya hewa. Hili ni janga la kidunia, tukiwa kama nchi ambayo ina misitu na maliasili nyingi yafaa tuendelee ku-maintain misitu, uoto wa asili, vyanzo vya maji, tusichanganye mifugo na wanyamapori kama ambavyo baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakichangia kwamba maeneo ya hifadhi nao wachunge ng‟ombe. Napinga vikali jambo hilo, tena nasisitiza sana kuwa sheria itumike ili waamue kupunguza mifugo na wakipunguza mifugo watafuga kwa tija badala ya sasa ng‟ombe kibao lakini ukiwatazama ng‟ombe hao wana uzito sawa na bata. Ni wazi kuwa ng‟ombe huyu hatamsaidia mfugaji, ni kero.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro wa kiwanda cha Baraghashi – Sao Hill. Hiki kiwanda kinapata gawio la misitu 60% bado wanapata bei punguzo. Jambo la kusikitisha ni kwamba kiwanda hiki kinazalisha karatasi ngumu, anasema finishing anakwenda kufanyia Kenya, jambo ambalo sio kweli, anachokifanya huyu mwekezaji ni kukwepa kodi ya Serikali. Nashauri afuatiliwe kwa ukaribu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) wafanye kazi yao badala ya kujiingiza kwenye biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia moja na naomba mchango wangu uingie kwenye Hansard.