Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa mchango wangu katika Wizara hii ya Maliasili na Utalii kwa kujikita katika suala moja.
Kwanza, napenda kuanza kwa kuunga mkono hoja katika Wizara hii ngumu, hususani upande majangili namna yanavyoipa wakati mgumu sekta hii ya maliasili na utalii, kitu ambacho kinapelekea kukosekana kwa watalii na ukosefu wa mapato kwa uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania leo tunazungumzia kukua kwa utalii kwa kuwa na watalii milioni mbili, wenzetu South Africa wanazungumzia watalii milioni 12. Hivyo basi, ni kwa Serikali yetu (Wizara) kuhakikisha inaboresha miundombinu ya maeneo yetu ya watalii. Kwa mfano, utalii wa Mlima Kilimanjaro miundombinu ya majitaka siyo mizuri kabisa hususan upande wa vyoo, vyoo ni vichafu. Mbaya zaidi vyoo ambavyo wanatumia wananchi/wafanyakazi wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ndiyo hivyo hivyo vinatumiwa na wageni wetu (watalii). Hii si sawa kabisa na ni moja ya sababu ya kufukuza watalii katika chanzo hicho cha Mlima Kilimanjaro. Sote tunafahamu wazungu/wageni ni waungwana na wasafi sana ukilinganisha na Watanzania wa maeneo yale. Hivyo basi, niitake Wizara kuhakikisha inajenga choo mahsusi kwa wageni wetu (watalii) na siyo kuwachanganya na wenyeji. Usafi ni sehemu ya kutangaza utalii wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni kuhusiana na mjusi aliyepelekwa nchini Ujerumani. Wabunge walio wengi wanahitaji mjusi huyo kurudishwa nchini, mimi naomba nitofautiane nao kidogo katika maana ya kwamba kuna gharama kubwa sana katika kumtunza, mjusi huyo aendelee kuwepo na kuingiza faida ya nchi. Kwanza ni mkubwa sana, hivyo anahitaji eneo kubwa sana, ni sawa na viwanja vinne vya mpira, lakini pia anahitaji muda wote kuwepo kwenye AC ili asiweze kuharibika/kuoza. Hivyo basi, kuliko kutaka arejeshwe sasa ilhali hatujajipanga, nipende kuishauri Serikali (Wizara) ni bora tuone utaratibu wa kuweza kupata royalty (mrahaba). Ni vyema Serikali yetu ya Tanzania ione utaratibu bora wa kuitaka Serikali ya Ujerumani kutupatia gawio linalotokana na utalii wa mjusi huyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, mchango wangu ni huo. Naomba kuunga mkono hoja.