Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuongelea kuhusu Operesheni Tokomeza. Kwa kuwa kulikuwa na Azimio la Bunge kwa wananchi walioathirika na Operesheni Tokomeza ni muhimu sana Serikali ikahakikisha inalipa fidia kwa wakati kwa wananchi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni kuhusu leseni ya biashara ya Nyara, kuna baadhi ya kampuni zilizopewa leseni hizo na baada ya muda leseni zikafutwa na tayari kampuni hizo zilishakuwa na nyara hizo na baada ya muda wahusika kukamatwa ilhali wakati wanatekeleza jukumu hilo walikuwa na leseni halali. Serikali itueleze kwa nini kumekuwa na mkanganyiko huu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, Wilaya ya Karatu inapakana na TANAPA (upande mmoja) na Hifadhi ya Ngorongoro (kwa upande mwingine). Wilaya imekuwa haina makubaliano ya kimkataba wa namna gani Wilaya hiyo inafaidika na utalii ili kujenga ujirani mwema. Misaada hiyo imekuwa inatolewa bila ya kuwa na uhakika wa kuipata (hisani). Ni kwa nini mamlaka hizi zisiingie makubaliano rasmi ya kimkataba ili Halmashauri iwe na uhakika kwa mwaka ni miradi ipi, kwa gharama ipi itatekelezwa na mamlaka hizo? Ni muhimu mambo haya yakawekwa wazi ili kujenga ujirani mwema.