Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mungu kwa kunipa afya njema na kuweza kuchangia hotuba hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwenyezi Mungu ameijalia nchi hii kuwa na neema na mali nyingi yapasa kumshukuru. Maliasili ya wanyamapori inaingiza faida kubwa ya Pato la Taifa kwa kuvutia watalii wa nchi mbalimbali na Serikali imepata pato la asilimia 25 siyo kidogo. Tunajua kuwa TANAPA inafanya kazi kubwa katika kuchangia pato kubwa katika sekta ya utalii katika nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya wakulima na wafugaji ni lazima Waziri wa Maliasili na Utalii akae na wenzake wa Wizara ya TAMISEMI, Kilimo, Mifugo na Halmashauri ili waende pamoja katika kutatua migogoro hii ili kuleta amani juu kwa wakulima na wafugaji na kuleta suluhisho la kudumu ndani ya nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya kihistoria yaliyomo katika nchi hii yaboreshwe ili tuzidi kuvutia watalii katika maeneo yetu kama vile Kilwa au kule Zanzibar sehemu ya Chwaka, Tumbe na maeneo mbalimbali ili tuzidi kuukuza utalii na kuzalisha kipato zaidi.
Kuhusu suala la mazingira hususani ukataji wa miti kwa ajili ya kutengeneza mkaa au kukata miti kwa biashara ya mbao vibali vinatolewa kiholela. Kwa kufanya hivi hii misitu itakwisha na ukame utashamiri katika nchi hii. Kwa hiyo, ni lazima Serikali iwe makini na kile wanachokifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango wangu huu, naomba kuwasilisha.