Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi. Pia nimpongeze Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais na Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa kuwa Waziri Mkuu. Nimpongeze Dkt. Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi sana na kuwa Rais wa Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Shaurimoyo kwa kunichagua mimi Mattar Ali Salum kuwa Mbunge wao, nawaahidi sitowaangusha.
Kuhusu kukabiliana na uamuzi wa kusababisha migogoro baina ya hifadhi zetu na watu wanaotumia kwa kulima au kufuga ndani ya hifadhi hizo, naiomba Wizara kukata mipaka na kugawa maeneo haya ili wakulima na wafugaji wapewe maeneo yao na kuweza kufanya shughuli bila ya kuingiliana na maeneo ya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie upungufu wa watumishi na vitendea kazi ni mojawapo ya tatizo kubwa linalosababisha kuzorotesha kwa maendeleo ya utalii. Naomba Wizara ifanye kila linalowezekana kuongeza wafanyakazi na kuwaongezea uwezo watendaji wa Wizara kwa kuwapa vifaa vya kazi ili kuweza kukabiliana na ongezeko la utalii. Pia kupata wafanyakazi ambao wanajua utalii kwa kuwa utalii ni moyo wa uchumi wa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kupangua kwa watumishi na vifaa vya kutendea kazi husababisha kushuka kwa idadi ya watalii nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uvunaji wa mkaa unaathiri sana ubora wa misitu. Naomba Serikali kupambana na wavunaji mkaa ili kuondoa na kupunguza matumizi ya mkaa. Naomba Wizara kuendelea kushirikiana na Wizara nyingine juu ya uuzaji na ukataji wa mkaa na kuongeza juhudi kuhakikisha wananchi wetu wanaacha kuchoma mkaa na kupunguza kwa sana matumizi ya kuni, mkaa na kuanza kutumia matumizi mbadala kama gesi na umeme. Pia Wizara iwashauri wananchi wetu wote kuanza matumizi haya. Naiomba Serikali iwashauri au kuwapa ushauri wananchi wetu kuacha matumizi ya mkaa ili kulinda misitu yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali ipunguze gharama za gesi ili wananchi waweze kumiliki matumizi hayo wenyewe. Bei iliyopo hivi sasa ni kubwa sana kiasi kwamba hupelekea wananchi wetu kushindwa kutumia gesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Wizara itoe mafunzo makubwa kwa wananchi wa vijijini ili waache ukataji wa miti ya kuchoma mkaa. Pia waache kupika kwa kutumia kuni na mkaa na waweze kutumia gesi. Nashauri Serikali kuongeza idadi ya pesa kwa kuongeza matangazo kwa kuwa sasa matangazo hayatoshi. Utengenezaji wa matangazo ndiyo sababu kubwa ya kukua kwa utalii wa nchi yetu na itazidisha mapato ndani ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutolewa kwa mafunzo maalum kwa watumishi wa sekta ya utalii kutasababisha kupanda hali ya uchumi na pia kutengeneza ubunifu wa maeneo mengine ili kuweza kutumika na sio kubakia na yaliyopo tu. Nashauri Serikali kuongeza maeneo mengine, hii ni mojawapo ya kukuza utalii nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Zanzibar, namshukuru sana Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Jumanne Maghembe, pia naishukuru Wizara ya Utalii Zanzibar kwa kazi nzuri wanazozifanya, na sasa utalii umekua sana, watalii wanaongezeka kuja Zanzibar, na ni watalii wengi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba ya Wizara ya Maliasili na Utalii.