Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hoja iliyoletwa mbele yetu. Aidha, baada ya kuunga mkono hoja naomba nichangie baadhi ya maeneo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mara nyingine ikiwa ni mara yangu ya nne kuongelea suala zima la maporomoko ya Kalambo pamoja na Hifadhi ya Msitu wa Kalambo kuwa chini ya TANAPA nimekuwa nikileta ombi hili na nitaendelea kurudia nikiamini ipo siku Serikali itanielewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maporomoko ya Kalambo yako mpakani mwa nchi ya Tanzania na Zambia. Pamoja na maanguko ya maji kuwa mazuri sana upande wa Tanzania kuliko upande wa Zambia lakini kwa upande wa Zambia wameyatangaza maporomoko haya kwamba ni maporomoko ya pili Afrika baada ya yale ya Victoria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili linashindikana kutokana na uwezo mdogo wa Halmashauri ya Kalambo kwa maana ya uwezo mdogo wa kifedha na weledi katika tasnia ya utalii. Hivi ninavyoongea tembo wanaokadiriwa 17 mpaka 25 wapo ndani ya msitu wa Kalambo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Wizara kwa mara nyingine maporomoko ya Kalambo na Msitu wa Hifadhi ya Kalambo viwe chini ya TANAPA ili wahifadhi na kutangaza vivutio hivi vya utalii.