Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwapongeza Waziri na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kwa kazi nzuri wazozifanya. Aidha, nawapongeza watendaji wa Wizara hii kwa maandalizi mazuri ya bajeti. Pamoja na pongezi hizi nashauri yafuatayo:-
(i) Wakati umefika wa kuboresha utalii kwa Mikoa ya Kusini (Mtwara na Lindi) kwa kuwekeza fedha za kutosha kwenye miundombinu itakayowezesha watalii kufika maeneo hayo.
(ii) Mbuga za wanyama na hifadhi zingine zitangazwe kwa uwiano sawa badala ya kutangaza zile za Arusha na Mara.
(iii) Wilayani Newala kuna Shimo la Mungu na lina maajabu ya aina yake. Naomba Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri waende wakajionee ili waweze kuchukua hatua ya kuweza kukiendeleza kivutio hiki.
(iv) Mto Ruvuma una pwani yenye kilometa 156 ambazo zinafaa kwa ufugaji wa mamba kwa ajili ya vivutio, tutumie beach hii ipasavyo.