Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Suleiman Masoud Nchambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja sana. Awali ya yote nakushukuru. Vile vile nakupongeza kama walivyosema, akinamama nanyi mnataka haki sawa, lakini waliimba hawa waimbaji, hata wakati wa kutembea, akinamama mbele, akinababa nyuma. Kwa hiyo, bado tunawaenzi. Akinamama wa Tanzania endeleeni kufarijika kwamba Serikali inayosimamiwa na Chama cha Mapinduzi...
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, usiyashangae haya, ukienda kusoma Biblia Luka 6:38 utayakuta. (Kicheko/Makofi)
Maana kile ambacho wanakipanda hapa, ndicho ambacho watakivuna. Niliwaambia shemeji zangu wa Kigoma, namshukuru sana Mheshimiwa Zitto, huwa anatumia knowledge yake kuleta mambo ambayo yana mashiko kwa Watanzania; lakini shemeji zangu wengine wote hawajarudi humu ndani. (Makofi)
Niliwaambia Luka 6:38, kile mnachokipanda humu ndani, ndicho mtakuja kukivuna 2015 Oktoba. Kwa hiyo, wamekivuna na hawa wengine, wala usiwe na mashaka, maana katika safari ya mamba na kenge na mijusi wamo, wala usitie mashaka juu ya hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndicho ambacho kimetokea hapa kabla ya kuanza michango yangu kwa Mheshimiwa Lwakatare. Amemaliza dakika zake zote, hakusemea Manispaa ya Bukoba. Mimi ni Mbunge wa Jimbo Kishapu, nimetokana na watu shapu, Wilaya yangu ni Shapu, mimi mwenyewe ni shapu. Naleta mambo yangu humu kwa ushapu kwa ajili ya wananchi wa Jimbo…
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Shapu! (Makofi)
Kwa hiyo, Wabunge wengine humu wanasimama wanapoteza muda wao wanaongelea mambo ambayo hayahusu. Mheshimiwa Lwakatare amesema sana, lakini hajatetea wananchi wake. (Kelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nataka niwaeleze ndugu zangu Wabunge kidogo, kazi ambayo huanza juu kwenda chini, ni kazi ya kuchimba kaburi peke yake. Kaburi huanza kuchimbwa juu kwenda chini. Kazi nyingine zote huanzia chini kwenda juu. Kwa hiyo, hata sisi hapa, kama Bunge ambalo Watanzania hawawezi kuenea humu ndani, wametutuma Wawakilishi wachache, tuje tuwasemee kuhusu mambo yanayohusu jamii na Taifa letu. Kwa hiyo, kazi tutakayoifanya hapa, ni ile wanayosema Wazungu a journey of thousand miles starts with a single step to a thousand steps. Tunaanza na hatua moja, mbili mpaka tunafika 1000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo wanaobeza, lakini Mungu ameleta Mitume wengi sana, hakuleta Mtume au Nabii mmoja. Lazima, we still keep on learning through history. Mungu hakuleta Mtume mmoja, alileta mitume wengi na alikuwa na makusudi maalum. Nasi hapa Mabunge yatapita mengi, Wabunge watakwenda wengi, kwa sababu kazi za kibinadamu zinaendelea siku hadi siku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu, nataka niwaambie, maneno machache sana; mpango huu umeletwa humu Bungeni, kwa mujibu wa kanuni ya Kibunge ya kwetu ya 94; lakini yapo mambo yaliyosemwa hapa ni kwamba siyo sahihi jambo hili kuletwa kwa wakati huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwakumbushe, ukisoma kitabu chetu cha Sheria za Bajeti, 2015, Kifungu cha 20 naomba ninukuu: “The Minister responsible for planning commission shall prepare and lay before the National Assembly and the National Development Plan which shall be the basis for the preparation of the National Budget.” Kifungu hiki kinapelekea maandalizi katika sheria yetu ya 2015 ya kitabu chetu cha bajeti Kifungu na 26.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka tuwekane sawa. Hapa hatukuja kutekeleza jambo, tumekuja kuandaa Mpango. Waheshimiwa Wabunge tusimamame hapa kwa Utaifa wetu, tusimame hapa kwa vitabu vyetu vya kikanuni, sheria na kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu. Hata dini, ninaposimama mimi Muislam nasoma the Holy Quran nina-refer; Wakristo wanasoma Biblia na kwa sisi wengine tunaamini Taurati na Injili. Hivi vitabu tuvipitie sana. Tuko kwa ajili ya Watanzania walio wengi nje, tuko kwa ajili ya Utaifa wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu Na. 26, ni lazima tuliweke jambo hili sawa ili Watanzania walioko nje wasione tu tunawaburuza, tunakwenda hatua kwa hatua. Naomba ninukuu:
“The National Assembly shall on or before 30th June each year and after debating the National Assembly, approve the Annually National Budget of the Government for the next financial year, by the way of open vote and call of the name of each Member of Parliament.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge watashirikishwa mmoja baada ya mwingine katika Mpango. Hapa sisi tunatoa mapendekezo ya mpango. Nawaomba sana, wote tunatoka katika Majimbo hata wenzetu wa Viti Maalum, Majimbo yanaunganishwa, yanaletwa. Ni imani yangu, Chama changu, Chama cha CHADEMA na wengine, wanawaleta Viti Maalum pia ambao wanajua watasaidia wananchi wote na hasa akina mama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba nielekeze sasa michango yangu kwenye maeneo, kama ilivyo kawaida ya Mbunge sharp. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yoyote haiwezi kupiga hatua, ni lazima iwe na mipango ya kiuchumi, tena mipango na mikakati mathubuti. Katika maeneo ya mipango ambayo itatekeleza uchumi, maana suala lote hapa, wanasema Mheshimiwa Magufuli ameahidi wanafunzi bure; tunataka watu watibiwe bure, fedha zitatoka wapi?
Mheshimiwa Magufuli amekuwa mstari wa mbele kutaka kuibadilisha Tanzania hii iende katika uchumi wa kati. Mambo yafuatayo ningeomba sana Waheshiwa Wabunge tuyasemee sana. Jambo la kwanza ambalo Mungu ametujalia Watanzania ni rasilimali watu. Tuna rasilimali watu, tena Watanzania wenye nguvu na sifa ya kuchapa kazi.
Jambo la pili ambalo nikikumbuka sana Mheshimiwa Muhongo alikuwa akipigwa madongo sana siku za nyuma; leo sote mashahidi, Wabunge tunapishana Ofisi za REA na maeneo mengine kuomba umeme na mambo mengine ambayo yatasaidia kututoa sisi katika uchumi wetu huu wa kimasikini kutupeleka katika uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile ulinzi ni suala muhimu sana. Lazima mtu yeyote anapotaka kuwekeza awe ana uhakika, yuko salama, ana imani anapowekeza mambo yake yatakwenda vizuri. Ujenzi wa barabara zetu; wakulima wetu wanapolima wanasafirishaje? Katika gharama zipi? Ujenzi wa reli; eneo hili ni muhimu sana ndugu zangu naomba niwaambie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa yako mimi nimekuwa dereva wa bus; kwanza nimekuwa mpiga debe stand, nimebeba abiria mgongoni, nimekuwa dereva wa bus, nimekuwa dereva wa malori; najua gharama za kusafirisha mizigo; na sasa ni mwekezaji, tena mfanyabiashara mzuri tu, wala sina matatizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitaka kuendelea katika nchi yetu, lazima tuwekeze katika miundombinu. Moja, reli itatusaidia sana. Lazima reli yetu iboreshwe katika level ya standard gauge, wananchi wetu wasafiri on and off. Unaweza ukatoka Kigoma kwa shemeji zangu kule amagambo bukebuke wakaja Dar es Salaam, asubuhi akanunua bidhaa akarudi. Mambo ni meeza, sivyo shemeji zangu, Mheshimiwa Zitto! Mambo yamekwenda! Wale wa Mwanza unaweza ukatoka jioni Mwanza ukaenda Dar es Salaam na ukarudi kesho, bila kulala guest. Ile fedha itasaidia kusomesha watoto na kuanzisha ujenzi wa nyumba zako. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba katika mipango yetu, Waheshimiwa Wabunge tuungane, tuhakikishe tunapata reli ili kupunguza gharama za maisha ya Watanzania; lakini tusafirishe bidhaa zetu kwa urahisi. Atakayelima matunda leo; nenda South Africa ukaangalie reli walivyojenga; nenda Uingereza uone mambo yalivyokwenda. Mwalimu wangu hapa Mheshimiwa Ndassa, anajua. Mimi leo…
MWENYEKITI: Muda wako umekwisha Mheshimiwa!
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI Nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja wabheja, naunga mkono hoja. Kwa pamoja naomba… (Makofi)