Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja na nataka kuwaambia wenzangu Wabunge na wananchi tuipe muda Serikali, hii ni bajeti ya kwanza na ni bajeti mpya baada ya kutoka kwenye uchaguzi. Tumetumia gharama kubwa sana kuleta demokrasia nchini mwetu, tumetumia pesa nyingi sana mwaka wa jana, tuipe muda Serikali, the best is yet to come, nawaahidi mambo yatakuwa mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuunga mkono hoja naiomba Serikali i-revisit upya suala la kukata kodi kwenye kiinua mgongo cha Wabunge. Nia njema ya Serikali ambayo ipo, lakini Serikali naiomba i-revisit. Kwa wastani Wabunge tunalipa kodi kwa miaka mitano tuko Bungeni hapa takribani milioni 50, inafika, I stand to be corrected kama utaweza kunirekebisha, lakini kwenye hesabu zangu tunalipa almost milioni 50 kwa miaka mitano ambayo tunakaa hapa Bungeni. Kwa hiyo, naomba Serikali wajaribu kuitazama hiyo upya.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni la kuongeza kodi kwenye mitumba. Hili ni agizo la Afrika Mashariki, ziko nchi kwenye Afrika Mashariki zina viwanda vya nguo, sisi hatuna, hii ni ajira ya vijana wengi nchini mwetu. Hawa vijana wakihangaika na biashara zao wataweza ku-create disposable economy. Wakipata chochote na wao watanunua soda, watanua cement, watachangia kodi kwenye kipato ambacho watakipata kwenye kuuza nguo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali wai-revisit hii kodi mpya kwa kutazama namna gani ajira zitaathirika katika nchi yetu. Yako malalamiko wananchi wanasema sisi Wabunge tunasema kodi hii ya simu, mimi nasema ni sahihi iwepo na ndiyo njia peke yake ya Serikali ya kupata mapato ya ziada. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, transaction ya M-PESA nchini mwetu kwa mwaka ni trilioni 50, trilioni 50 transaction ya pesa zinazozunguka kwa mwananchi na mwananchi mwenzio ni fifty trilioni kwa mwaka. Makampuni haya yana-lobby kuona kuwa wanaoumia ni maskini, si kweli watakaoumia ni wao. Kwa hiyo, kodi hii naiunga mkono, Serikali iendelee na kodi zingine na kukamata mapato kwenye simu, we are losing a lot of revenue kwenye maeneo haya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye simu kuna non voice revenue, haya ndiyo maeneo Serikali inatakiwa ikae iyatazame. Pesa nyingi sana zinapatika kwenye non voice revenue ambayo sheria zetu hai-capture, inafanya makampuni haya yanaondoka na hela nyingi. Mfano mdogo, Kenya walilalamikia wananchi, lakini Kenya they put their foot down kodi ile ye transfer imewekwa na leo M-PESA, Safari com peke yao wameongeza wateja 21 percent kama hii inaumiza wananchi Kenya wangesema.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wetu na sisi tubadilishe minding setting zetu, Waheshimiwa Wabunge tusiwe na tabia ya kizamani ya kuona tukilipa kodi watu wanaumia, bila kodi Serikali hii haichapishi note. Simu hizi unakaa Dar es Salaam unapeleka pesa Jimboni within second hivi kulipa hata shilingi 400, 500 kwa kila transaction tatizo liko wapi? Ukienda Ulaya Dollar to Pound shilingi ngapi tunakatwa, ukienda Ulaya Dollar to Euro shilingi ngapi tunakatwa, commission za bureau de change, kwa nini tunaogopa kulipa kodi za Serikali? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Kenya, Safari com peke yake imepata faida ya six hundred billions kampuni moja, sisi Makampuni yetu miaka yote yanapata hasara. Kwa hiyo, Serikali put your foot down, kamata hizi kodi ili wananchi wapate huduma. Pia regulator TCRA lazima wajue teknolojia inavyobadilika business as usually imekwisha, wawe on their toes kuhakikisha makampuni haya yanalipa hizi kodi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye extractive industry transparency initiative kwenye madini. Nchi yetu ni ya tatu katika ku-export gold lakini utajiri huu haurudi kwa watu, haurudi kwa watu kutokana na baadhi ya policy zetu ambazo haziumi. Leo Tanzania katika nchi 182 ni wa 152 katika human development index, this is wrong. Haiwezekani nchi yenye madini kama haya tuwe 152 katika nchi 185 katika human development index.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka 2010 Tanzania ime-export trilioni tatu na bilioni mia tatu ya dhahabu, pato la Serikali mpaka 2010 was only seven percent, bilioni 220. Hii inatokana na matatizo ya multinational corporate, misinvoicing, ku-abuse transfer pricing. Kama Serikali tunazo policy nzuri lakini tunakuwa tuna-mismanage eneo hili sababu ya under staff na capacity ya watu wetu kuweza kujua hivi vitu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2002 mpaka 2011 tumepoteza trilioni 18, eighteen trillion kwa misinvoicing, makampuni haya wajanja sana wa kuleta mitambo mikubwa kudanganya bei ambazo watu wetu hawana capacity ya kujua. Kwa hiyo, naiomba Serikali badala ya kuingia kwenye VAT za tourism, kamateni hela huku. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, abusing ya transfer pricing bado ipo, share zinauzwa, mamlaka zinazohusika hazifuatilii, lingine adhabu kali tunazo, zitumike.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna conversion on mutual administrative assist in tax kama Serikali imesahau Waziri wa Fedha ataniambia hebu ai-note hii kitu na Mwanasheria Mkuu yuko hapa. Conversion on mutual administrative kwenye kodi, hiki chombo hatuja ki-sign, kama tumeki-sign na kwa vile hatukukisaini hatupati information ya makampuni haya ya disclosure za kodi zao kwenye nchi zao. So we are losing money simply sababu hatuja-sign huu mkataba, tuki-sign huu mkataba tutasaidiwa kuambiwa kampuni fulani ina- disclose nini kwenye nchi zao.
Kwa sababu nchi zao wameweka sheria lazima u-disclose activity unaifanya kwenye foreign country ili na wao waweze kubana kulipa kodi, kama imefanywa fine kama haijafanywa kwa nini haijafanywa? Inawezekana haikufanywa au imechelewesha kufanywa kwa sababu mambo haya tunafahamu ya mishemishe ambayo kila mtu anayajua, lakini with this Government kama haijafanywa ifanywe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni shida kubwa sana, lakini niipongeze Serikali kwa kuwa na mpango wa Sovereign Wealth Fund kwenye gas and oil. Wenzetu Trinidad na Angola wamefanikiwa kwenye rating za confidence za investors. Wameweza kuweka five billion kwenye accout zao za mfuko wa baadae wa vizazi vyao kwenye Sovereignty Fund za nchi zao, inaleta confidence, inapunguza inflation ya pesa zetu ambazo tunazipoteza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, TMAA, auditors wa Madini wanafanya kazi nzuri sana nchini lakini TRA wanatakiwa wawe zero distance na hawa watu ili wanapotoa ushauri waende wakakamate kodi kwenye extractive industry.
Nakushukuru naunga mkono kwa asilimia mia moja.