Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata fursa hii. Pia niwashukuru wananchi wa Manyoni Mashariki kwa kura zao nyingi, kwa imani yao kubwa kwangu mimi mpaka kuniingiza katika Bunge hili Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema, nimepitia mapendekezo ya mpango huu, nimeyapitia vizuri sana, nikiitazama nchi yangu Tanzania, nikiwatazama Wabunge wenzangu humu ndani kama Wawakilishi wa wananchi. Mpango huu nimeuelewa vizuri, sijaona mahali pabovu. Ni sisi tu Wabunge kujazia nyama ili Mheshimiwa Waziri wa Fedha na timu yake, waende sasa kuuandaa vizuri kwa ajili ya kuja kuuwasilisha kipindi kijacho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kabla hata ya Mpango huu kuanza naona gari limeshaanza kuondoka na ninahisi gari hili kasi yake itakuwa kubwa. Nikimtazama dereva aliyepo ndani, Dkt John Pombe Magufuli ni dereva mahiri ametia imani Watanzania, gari litakwenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huu, naomba niende moja kwa moja kwenye mjadala. Baada ya kuupitia mpango huu, kuna vitu na mimi kama Mbunge ambaye ni moja ya kazi zangu naomba sasa nijazie. Mpango huu ni mzuri, utatuvusha kama tutayazingatia yote hayo. Kila mmoja kama akitimiza wajibu wake Waziri kwa maana ya Serikali watimize wajibu wao kwa kutenda na sisi tutimize wajibu wetu katika kushauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona kuna kipengele cha sheria, tukitazame kwa makini. Kuna sheria nyingi ambazo zinahitaji marekebisho, sheria zile ambazo zinagusa mpango huu. Sheria kwa maana ya sheria zile Principle Legislations, Sheria kubwa lakini pia sheria ndogo kwa maana Subsidiary Legislations, nikizitazama naona nyingi zina upungufu. Hazitakwenda na kasi ambayo Mheshimiwa Rais na Serikali yake ambayo naiona ni kubwa ni lazima kama Wabunge tuzitazame sheria hizi. Kuna Kamati zimeundwa, kuna Kamati ya Sheria na Katiba. Naomba wakae chini watizame sheria zote zinazogusa mpango huu, tafadhali sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sheria ya Manunuzi ya Umma namba Saba ya mwaka 2011, sheria hii imeijeruhi sana nchi yetu, sana tu. Naomba iangaliwe upya, Kamati hii ilete mapendekezo baadaye Waziri mhusika ailete, kama ni kurekebisha turekebishe, kama ni kufuta na kuandika nyingine ifutwe na tuandike nyingine, naomba tuiangalie ni sheria mbaya kabisa, sheria inayoruhusu kununua vifaa chakavu, sheria inayochukua mlolongo mrefu kwa muda kidogo tu. Kwa mfano, kujenga nyumba, jengo labda la ghorofa mbili, inachukua karibu miezi sita. Tunakwenda kwenye uwekezaji, tunakwenda kwenye kujenga viwanda, lazima sheria hizi ziwe rafiki, zichukue muda mfupi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa. Mpango huu unatajwa kuinasua nchi kwenda kwenye kipato cha kati, bila kuja na sheria mahiri ya kuzuia na kupambana rushwa, tutakuwa tunatwanga maji na kuishia kulowa. Naomba sheria hii pia ibadilishwe, irekebishwe, hatuwezi kuendelea kuvumilia baada ya jalada la uchunguzi kukamilika, liende kwa DPP, ofisi inayojitegemea, Mkurugenzi wa TAKUKURU hawezi kumfuatilia huyu, kuhimiza kwamba muda ni mfupi, inachukua muda mrefu, hatuwezi kufika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama Maalum imetajwa, sheria hii itakapoundwa maana yake Mahakama Maalum kwa ajili ya makosa ya rushwa tu lazima iundwe. Nazigusa Sheria ziko sheria nyingi, Sheria za Uwekezaji, milolongo mirefu na regulations zake zina milolongo mirefu sana zinafukuza wawekezaji, lazima tuweke mazingira rafiki kwa wawekezaji wetu.
Niguse maeneo wezeshi kidogo tu angalau. Upimaji wa ardhi; hatuwezi kuzungumzia viwanda bila kupima ardhi zetu, hatuwezi! Tutumie wataalam tupime ardhi zetu. Tuainishe maeneo, maeneo ya makazi, maeneo ya viwanda, maeneo ya biashara, lazima tutenganishe. Huu ndugu zangu ndiyo ustarabu wa mwanadamu, planning. Tutumie wataalam wetu tu-plan, tu-plan Miji yetu, tuiangalie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa Mbeya, nilipita Kibaigwa hapa, kuna Mji mmoja unaitwa Tunduma, ka-centre kamoja kanakua kwa haraka sana. Ukiangalia nyumba zilivyomwagika kama takataka. Inaondoa ustaarabu wa mwanadamu. Tunao wataalam, tupime miji yetu. Msongamano wa Tunduma ule kama Mji ungekuwa umepimwa tusingekuwa na msongamano kama ule. Kibaigwa ule ni mji mmoja mzuri sana, lakini kama ungepimwa viruzi, ule mji ni ungekuwa ni mzuri sana. Tutumie wataalamu sasa wetu, kupima miji yetu. Pia kupima inasaidia kukusanya mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kushauri pia kwenye suala hili la mapato kwa maana ya kukusanya kodi. Hebu tuunganishe ukusanyaji wa kodi za majengo na ukusanyaji wa kodi za ardhi zilipwe katika eneo moja. Tutumie wataalam wetu wapo, GIS kwa maana Geo Information System nzuri kutambua maeneo na kuweza kukusanya kodi kwa urahisi kabisa. Tunayo deed capital kwenye majengo haya, kubwa mno kama tutatumia wataalam tutaweza ku-realise mapato makubwa sana ya kugharamia mpango huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nigusie kidogo suala la utalii. Utalii pia ni chanzo kimoja kikubwa cha mapato yetu. Sisi Manyoni pale, Jimbo la Manyoni Mashariki tunalo eneo linaitwa Kilimatinde, eneo hili linavuma sana kwa umahiri kwa kumbukumbu nzuri ya mambo ya kale. Ukipita pale Manyoni kuna njia ya Watumwa ambao walipita karne ya 18. Tangu karne ya 18, pale alipokanyaga mtumwa mpaka leo hapaoti jani wala mti.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Daniel Mtuka muda wako tayari.