Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kabla sijachangia nikiri kwamba mimi ni mfanyabiashara wa utalii kwa takribani miaka 12 sasa kwa hiyo ni field yangu ya experience.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachangia kwa masikitiko kwa kiasi fulani, wengi wamezungumza hapa kila mmoja anafahamu ni kwa kiasi gani nchi yetu ni nzuri, iko kwenye at least top ten za dunia, lakini tumekaa hapa tunashangilia, wakati fulani Wabunge huku walipiga makofi kwamba tumefikia watalii milioni moja. Watalii milioni moja ni wachache mno, sana kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi kama South Africa ambayo tuko equally beautiful I would say. Wanakwenda sasa hivi watalii milioni 12 kwa mwaka, Misri wako milioni 15, wakati ule kabla hawajagombana sijui sasa hivi iko ngapi. Nchi kama Thailand nazungumzia nchi ambazo hazina uchumi mkubwa kama sisi, wana watalii milioni 25 kwa mwaka, Indonesia, Singapore milioni 15; Tanzania watalii milioni moja tunashangilia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wakati sasa umefika tufanye jitihada za maksudi kuhakikisha kwamba tunanyanyua kiwango hiki cha watalii wanaokuja Tanzania, kiukweli kama sasa hivi wanakuja milioni moja tu wanachangia asilimia 17 ya GDP yetu wangefika milioni tano ingekuwaje, kwa mfano? Ingekuwa ni zaidi ya nusu ya GDP; kwa maana hiyo ingeweza ku-observe shock zote hizi za matatizo ya ajira kwenye Taifa letu, ningekuwa nina mamlaka ningeweza kusema kwamba Serikali yenu hii ya sasa angalau ingechukua vitu vitatu comprehensively. Ingechukua viwanda vya Mheshimiwa Mwijage kama anavyokuja navyo vizuri; amejipambanua vizuri Mheshimiwa Mwijage kwenye viwanda, mchukue Mheshimwia Mwigulu kwenye kilimo, mifugo na uvuvi, ukaweka na utalii hapo tunaweza kuchukua watu wengi ambao hawana ajira katika Taifa letu tukawa-absorb kwenye maeneo haya. Hivyo, ningeshauri tu kwamba tuangalie ni sababu zipi zinapelekea Taifa letu kukosa watalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uzoefu nilionao mimi, nimekwenda kwenye trade fair za kutosha na watu wa Mheshimiwa Maghembe wa TTB nimekwenda nao na nina masikitiko makubwa sana kusema kwamba watu wetu wa TTB wanakwenda kwenye trade fair kupumzika, hawaendi kufanya kazi ukilinganisha na mataifa mengine ambayo tunayakuta kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata nilivyosikia mmewanyang‟anya sijui fungu mmelipeleka wapi niliona ni sawa tu, kwa sababu wenzetu wale wanakwenda kupumzika hawaendi kutafuta biashara, mara nyingi nimekwenda nao kwenye masoko mbalimbali nje ya nchi. Kwa hiyo, niseme kwamba tuangalie tena ni maeneo gani ambayo mojawapo ni kwamba Tanzania ni destination ambayo ni very expensive, ni ghali mno kuja Tanzania ukilinganisha na kwenda maeneo mengine ambayo naona watu wanaweza wakawa wanavutika kwenda kutalii maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tu-review tena hizi sababu ambazo zinasababisha tuwe ghali. Kwa mfano, airport zetu wanasema handling fees ni mojawapo inayosababisha tiketi ziwe ghali kwa watalii wanapotaka kuja Tanzania. If that is the case na kwamba kweli tunataka ku-promote utalii Tanzania tufike hiyo namba ya watalii ambayo mmeiweka target kwa sasa hivi ambayo ni milioni tatu ambayo naiona ni wachache, tuangalie hivi sababu vidogo vidogo, handling fees, airport departure taxes zile mnazi-regulate vipi ili kupunguza gharama ya mtu kuja Tanzania, maana yake mtalii anapokuja tusizungumzie ile package tu ambayo anailipa kuja kufanya utalii, lakini zungumzia pia na fedha anazokuja nazo mfukoni nyingi ambazo Watanzania wengi huko mitaani wanazisubiri kuuza bidhaa zao, vitu mbalimbali ambavyo wazungu wanavinunua. Tena wanavinunua kwa kusema mzungu price, tourist price, siyo kama wengine. Sisi tunakunywa soda shilingi 600, shilingi 700; mzungu anakunywa kwa shilingi 2000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakifika milioni tano ina maana kutakuwa na dola nyingi ambazo tutazi-retain hapa, ambazo zimekuja indirect. Kwa hiyo, tuangalie mapato ambayo ni indirect, mtalii anaweza kutuletea. Kwa hiyo, tujaribu kuwa-entertain waje kwenye nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine vitu vingine vinavyosababisha tukose watalii wa kutosha, kuna hizi issue za viza, tusishindane na Uingereza, Ufaransa sijui na ninyi mnapokwenda kutembea nje mnalipa viza kubwa. Muingereza aki-charge laki mbili kwenda Uingereza, tusishindane nao kwa sababu wale wanapokea watalii karibu milioni 50 kwa mwaka, sisi watalii 1000! Kwa hiyo, tuangalie namna gani tunawa-entertain kupunguza mzigo ili hawa watu waje wakishafika hapa ndiyo tutajua jinsi ya ku-deal nao, mnafahamu pia kwamba mtalii anapofika hapa anachukua precautions nyingi sana.
Mheshimiwa Waziri, nisikitike kwamba figures ambazo umetupa hapa za watalii waliokuja mwaka jana siyo sahihi. Utalii mwaka 2014/2015, ume-drop kwa zaidi ya asilimia 50 mzee. Ugonjwa wa Ebola ilitu-affect sana na tumepunguza wafanyakazi sana kwenye makampuni yetu huko Arusha. Niseme tu kwamba ukitaka kufanya uhakiki vizuri wa hili jambo kesho kutwa week end inayokuja kuna Karibu Fair, nenda pale utawakuta wadau wa utalii, wahoji, waulize biashara ilikuwa vipi bila kujali ninyi mmekusanya kiasi gani, kwa sababu kuna mbinu nyingi za ninyi kukusanya mapato, kwa hiyo, utalii uli-drop sana, toka Ebola ilivyozuka, tulipoingia kwenye uchaguzi pia watalii wanatabia ya kutotembelea nchi, lakini ninyi rekodi zenu zinasema ni 80 percent, siamini kama hiyo ni sahihi na tukafanye utafiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wazungu wanapokuja, sorry kule Arusha tumezoea kusema wazungu, badala ya kusema watalii. Watalii wanapokuja wanameza dawa za malaria, lakini pia kwa baadhi ya nchi wanapofika airport wengine kama hawajadungwa sindano, wanandungwa sindano ya yellow fever, pale panatokea kizungumkuti kikubwa sana unajua siyo kila mmoja anapenda kudungwa sindano, wakija pale maafisa walioko pale wengine hata kwa yale mataifa ambayo hayatakiwi kudunga hizo sindano wanakamatwa wanakuwa harassed, wakati mwingine hongo zinatembea wanaingia bila kudungwa hizo sindano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niseme kwamba tufanye overhaul ya marketing strategies zetu tukafanye kazi. Ningeshauri kwamba yale mataifa ambayo ni makubwa yanaleta utalii kama Ujerumani, Uingereza, Canada, USA nimesema, Japan tuseme na China; kwanini tusifungue ofisi kule na tukawapa watu kazi na wapewe target ya kuhakikisha kwamba wanaleta wageni Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wachina ni watu ambao wana uchumi mzuri sana sasa hivi lakini kiukweli tumeshindwa kuwa-reach kwenye soko lile. Pamoja na kwamba kweli tunataka kujilinda wenyewe hapa ndani kwenye suala la utalii wawekezaji kutoka nje ni muhimu sana. Kuna matatizo ya lugha na connection, tukisema kwamba sisi wamatumbi hapa ndiyo tuifanye tu peke yetu hatutafikia hiyo target.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo Immigration waangalie namna gani tuna collaborate na hawa watu wanaotoka nje, maana hawa ndiyo wana access na masoko ya kule kwao. Tuwarahisishie utaratibu wa kuingia hapa na wao watakapoleta wageni wakifika hapa kwetu na sisi tutapona hapo. Lakini tukisema tufanye wawekezaji wa ndani na nini? Kumchukua mzungu kutoka ya kuwekeza kwetu, tuwawekee mazingira mazuri, na yawekwe rahisi kama Rwanda wanavyo fanya, Tanzania tumekuwa na bureaucracy kubwa sana, ningeshauri kwamba tuangalie hivyo.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Airlines, pamoja na kwamba mnakwenda kununua ndege zenu ambazo ni chache kwa kweli na ningeshauri pia kwamba tununue na zile ndege ndogo kama hizi za Precision Air - HR kwa ajili ya kuweza kuhudumia viwanja vyetu vidogo vidogo hapa ndani, kulikoni kuwaachia private sectors ambao flight charges zao ni ghali sana. Kutoka tu Arusha kwenda na kurudi Serengeti shilingi 800,000. Kwa hiyo, tuwe na ndege za Serikali au ambazo tunaweza tukawa na ubia ili tuweze ku-regulate price za fares. Tuweze kutoa wageni Arusha kuwapeleka Ruaha, Katavi na maeneo mengine kama Mikumi, kufanya hivyo sasa hivi ni tatizo, mgeni akileta enquiring kwenye makampuni yetu anataka kwenda Kusini na sisi tuko Kaskazini huwa hatufanyi hiyo biashara, kwa sababu ya jinsi ya kufika kule gharama ni kubwa sana na pengine kwa sababu ya uchache wao tunakuwa hatuna contacts. Kwa hiyo, tuboreshe maeneo hayo ili tuweze kutanua huu uwigo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini airlines za kimataifa…
MWENYEKITI: Ahsante sana.