Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ili nami niweze kuchangia hotuba hizi mbili alizozileta Waziri wa Fedha na Mipango, Hali ya Uchumi na Bajeti ya Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetujalia uzima na salama, leo tumekutana hapa kujadili mambo yanayohusu mustakabali wa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumshukuru sana Dkt. Phillip Mpango, Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji kwa kutuletea bajeti ambayo nimeiita ni bajeti ya kihistoria. Haijapata kutokea katika historia ya nchi yetu Bajeti ya Maendeleo ikawa asilimia 40 ya bajeti yote ya Taifa. Kwa kweli pongezi nyingi sana zimwendee Mtukufu Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa dhamira hii ya dhati ya kuwaondoa wananchi wa Tanzania katika lindi la umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, napata faraja kubwa sana, nilikuwa najaribu kufanya tathmini ndogo hapa, nikagundua miundombinu peke yake imetengewa asilimia 25.4, elimu asilimia 22 na bajeti ya afya ni asilimia 9.2. Hapa kwenye bajeti ya Wizara ya Afya, Abuja Declaration inatutaka tutenge bajeti ya asilimia15. Wanasema Rome haikujengwa siku moja, kidogo kidogo ndani ya bajeti mbili, tatu zijazo tunamwomba sana Dkt. Mpango Azimio hili la Abuja la asilimia 15 katika bajeti ya Wizara ya Afya lifikiwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, nijielekeze moja kwa moja kwenye kuchangia bajeti. Ushiriki wa sekta binafsi na sekta ya umma katika miradi ya pamoja kimekuwa ni kilio cha siku nyingi sana, tumelizungumza sana hili na ninayo furaha na nahisi faraja kubwa sana, kupitia kwenye bajeti hii nimeuona ushiriki huu wa sekta binafsi na sekta ya umma kwa maana ya PPP, tatizo langu ni dogo tu!
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha basi atuletee na mchanganuo, kwa sababu tumeona tu humu miradi, mimi naiona kama ni blanket imewekwa humu, miradi kama ya barabara ile ya Chalinze – Dar es Salaam express way, mradi wa Reli ya Kati, miradi hii ya umeme ya phase III kule Kinyerezi ipo tu kwa ujumla ujumla!
Mheshimiwa Naibu Spika, tungeomba sana hebu watupatie break down na frame work, timeline kwamba miradi hii tunafanya labda tutaanza na mradi wa reli ya kati standard gauge, labda tarehe fulani mpaka itakapofikia mwaka wa fedha miaka miwili, mitatu, mbele mradi huu utakuwa umekwisha; labda mradi wa bandari ya Bagamoyo utaanza tarehe fulani mwaka wa fedha fulani na utakwisha hivi, ili tupate kwa ujumla wake haya mambo yanakwendaje; lakini kutujazia tu miradi ya jumla bila ya kutupa timeline inatusumbua sana, kwa sababu tunajenga matumaini, lakini ndani yake hatujui miradi hii itakuja lini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nijielekeze kwenye suala la utalii. Nilizungumza hapa kwenye Wizara ya Maliasili na Utaii ilipoleta bajeti yake na nashukuru sana Mheshimiwa Waziri namwona pale na namwomba Mheshimiwa Waziri anitegee sikio. Takwimu zinatuambia kwa miaka miwili kati ya mwaka wa fedha uliopita na mwingine wa nyuma yake, utalii wetu umeshuka kwa karibu watalii laki moja, sasa sitaki kujielekeza kwenye sababu gani zimepelekea watalii kupungua. Nataka nijielekeze kwenye namna ambavyo tunaweza tukatangaza utalii wetu ili tupate watalii wengi na kuhakikisha kwamba tunapata mapato katika Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, unapozungumza utalii mara nyingi tunajikita kwenye vitu viwili tu, Mlima Kilimanjaro na Mbuga, wakati Tanzania na Naibu Waziri wakati anajibu swali hapa juzi alisema wazi kwamba Tanzania ni ya pili duniani kwa vivutio vya kitalii, sasa hivi vivutio vingine vitatangazwa lini?
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi natokea Kisiwa cha Mafia na nilizungumza hapa wakati wa bajeti ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii kwamba kule Mafia tuna samaki anaitwa ‗Papa Potwe‘, huyu samaki ni samaki wa ajabu, anatabia kama za dolphin, ni samaki rafiki, watalii wanapenda sana kuja kuogelea naye. Je, ni wangapi wanajua habari za samaki huyu ‗Papa Potwe‘?
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana tunaomba sana mtengeneze package ya vivutio vyote ili muweze kwenda kuviuza huko nje, kwa sababu Halmashauri hatuna uwezo wa kumtangaza ‗Papa Potwe‘! Ni lazima tusaidiwe na nguvu ya Serikali. Kwa hiyo naomba sana tutanue wigo katika utalii wetu katika kuutangaza na kuhakikisha kwamba tunapata mapato mengi ili kuendeleza nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri wa Fedha Dkt. Mpango, hili nililizungumza kwako kama mara moja au mara mbili hivi, masikitiko yangu makubwa kuona kwamba Kisiwa cha Mafia hakikuingizwa katika zile flagship project kwa ajili ya Mpango wa Pili wa Maendeleo, kwa maksudi kabisa! Mimi nilikuwa naiona Mafia kama ndiyo Zanzibar mpya! Tuifungue kiutalii Mafia ili watalii waje.
Mheshimiwa Naibu Spika, pale tuna matatizo mengi na tunahitaji investment ndogo sana kuifungua Mafia. Barabara inayotoka Kilindoni mpaka Rasimkumbi kilometa 55 ikitengenezwa hiyo ikitiwa lami pamoja na bandari yetu na ndugu yangu Ngonyani pale ananisikia, kuhusu bandari ya Nyamisati, Mamlaka ya Bandari imetenga nafahamu kwamba bilioni 2.5 kwa ajili ya ujenzi wa bandari ile, ikikamilishwa sambamba na bandari ya Kilindoni na kuongezwa kwa runway, airport ya Mafia…
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja.