Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi pia niweze kuchangia Hali ya Uchumi na Bajeti ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Naibu wake pamoja na wasaidizi ambao amefanya nao kazi bega kwa bega na hatimaye kutuletea kitu kamili na kilichoiva vizuri cha namna hii kwenye Bunge lako Tukufu.
Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Serikali kwa nia yake ya dhati kutaka kutuelekeza kwenye kujitegemea kama Taifa, kwa sababu ukiangalia bajeti ilivyotengenezwa, na hata maelezo yake ambayo yamesomwa na Mheshimiwa Waziri kwa kweli yanaonesha dhamira ya Serikali kujitegemea na yanaonyesha ya kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kabisa kupeleka maendeleo kwa wananchi baada ya kutenga asilimia 40 ya bajeti yake kwenye fedha za maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kutoa mchango wangu kwa kuangalia mambo mawili tu kwenye hali ya uchumi. Jambo la kwanza ni lile la kujitegemea kwa kuimarisha viwanda kwa ajili ya uchumi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwezeshaji wa suala hili unategemea uwekeshaji na tunapozungumza juu ya uwekezaji huu maana yake tunamzungumza mtu mwenye mtaji wa hapa ndani na mwenye mtaji wa nje ya nchi yetu. Lakini nadhani ni jambo moja tu ambalo limewekewa nguvu sana katika kuhakikisha kwamba tunapokuwa na uchumi wa viwanda tunatengeneza ajira na hatimaye tuweze kukusanya kodi, huo ni upande mmoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna upande wa pili ambao naona kama tunausahau kidogo; kuwawezesha hawa Watanzania, hasa wakulima wetu wadogo wadogo ili na wenyewe wajumuishwe kwenye harakati hizi za kuinua uchumi wetu wa viwanda kwa wao pia kushiriki, si tu kuzalisha malighafi, sio kuwa vibarua au kulipwa mishahara au kuajiriwa kwenye viwanda au kwa wawekezaji; lakini wao pia kushiriki kama wawekezaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimejaribu kuangalia ninaona kuna pengo kubwa sana. Wazalishaji wetu wadogowadogo, hasa wakulima wanaunda nguvukazi ya asilimia 65 na kutokana na taarifa mbalimbali, wanatuzalishia malighafi za viwandani, wanatuzalishia chakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwenye harakati zetu hizi za kujenga uchumi wa viwanda tunawaangalia kama waajiriwa peke yake, hatujawaangalia kama watu ambao wanaweza wakaja pamoja na wao pia wakashiriki kama wawekezaji, wakaendelea kuzalisha kama ambavyo wameendelea kuzalisha toka uhuru wa nchi hii. Wamezalisha wametupa chakula, wamezalisha wametupa malighafi za viwandani, wamezalisha wametupa mazao ambayo tukiuza nje tunapata fedha za kigeni. Sasa nilikuwa najaribu kuangalia Serikali imeweka mkakati gani jumuishi ili na wao waweze kushiriki kwenye uwekezaji huu ambao tunataka nchi yetu tuwekeze halafu hatimaye tuwe nchi ya kipato cha kati.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushirika wa wakulima hawa wadogo wote tunafahamu umekuwa hauna nguvu sana ni dhaifu sana. Mimi nilikuwa nafikiri kama ungetiliwa nguvu ungekuwa una nguvu za kutosha kuweza kutumika kuwafanya hawa wazalishaji wadogo wadogo ili wao wawe wawekezaji kwenye maeneo yao. Wamekuwa wawekezaji kwa muda mrefu sasa Serikali inatengeneza mazingira na kuweka mkakati gani ili kuwafanya hawa watu badala ya kutoa tu nguvu zao, badala ya kufanywa kama wafanyakazi na wenyewe wawe wawekezaji kwa namna ambavyo wamekuwa wawekezaji toka mwanzo?
Kwa hiyo nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri atakapojumuisha ajaribu kutufafanulia, kwamba hawa wakulima wadogo wadogo hasa wakulima wadogo wadogo wa wa vijijini wana wekewa mazingira ya namna gani ili na wenyewe waendele kuwa wawekezaji wadogo wadogo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni suala la thamani ya shilingi yetu, zimetajwa sababu zinazofanya shilingi yetu iendelee kuporomoka. Moja ni kuimarika kwa dola ya Kimarekani, lakini lingine ni kuchelewa kupatikana kwa fedha za kigeni hasa kwenye bajeti yetu, pia mapato kidogo ya fedha za kigeni. Lakini kuna moja ambalo tunaona na wachangiaji wengine wamekuwa wakilitaja hapa, la hawa watoa huduma pamoja na bidhaa kutaka kupata malipo kwa njia ya dola, halijatajwa hata kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili pia limekuwa kero kwa wananchi hasa wa kawaida na wananchi wengine kwamba ukitaka kununua bidhaa au ukitaka kununua huduma ulipe kwa dola. Suala hili nalo linasababisha thamani ya shilingi yetu kushuka. Kwa hiyo na lenyewe Mheshimiwa Waziri angetusaidia ni kwa namna gani Serikali inakuja na uamuzi uliothabiti na ulio wazi, kwa sababu sheria ipo inayozuia jambo hili lakini bado linaendelea.
Mheshimiwa naibu Spika, suala lingine la tatu ni hili linalohusiana na shilingi milioni 50 kwa kila kijiji. Naipongeza Serikali kwa sababu imeanza kwa kutenga shilingi bilioni 59 ili kwamba ziende kwenye vijiji zaidi ya 1000 kwenye nchi yetu yote. Hapa bado kuna kizungumkuti kwa sababu Serikali inasema itapeleka pesa hizi kwenye SACCOS, sasa najaribu kujiuliza hizi SACCOS ambazo zitapelekewa hizi pesa Serikali inazifahamu na kama inazifahamu hizi SACCOS ziko kila kijiji? Maana vijiji vingine havina SACCOS, hii hela itapelekwa kwa nani? Kwa taasisi ipi ili iweze kuzitoa hizi pesa kama mikopo kwa watu wetu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nilikuwa na mapendekezo kwenye jambo hili. Mimi nilikuwa nafikiri badala ya kutegemea SACCOS ambazo hatujazitathmini na hatujui kama ziko kila kijiji, kwamba badala ya kufanya hivyo tungeunda Bodi za Mikopo za Vijiji vile ambavyo vitapelekewa hizi pesa. Bodi hii ya mkopo iwe ndiyo inasimamia hizi pesa kujaribu kuzigawa au kuzitawanya kwenye vikundi au kwa watu ambao wako kwenye vikundi ili kupata hii mikopo lakini kwa riba nafuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa napendekeza kwamba hizi fedha ziwe ni revolving au ziwe za mzunguko; kwa sababu mpaka sasa hivi hatujaelewa kwamba zitakuwa ni za namna gani, maana zikienda kwenye SACCOS hauziiti tena za mzunguko.
Kwa hiyo, nilikuwa nafikiri ziwe za mzunguko, na hizi pesa zibaki kwenye kijiji husika zisiende kwenye vijiji mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nilikuwa napendekeza kwamba usimamizi wa hizi bodi ufanywe na Maafisa Maendeleo wa Kata na Maafisa Maendeleo wa Wilaya zetu na hizi shilingi bilioni 59 wakati wakuzigawa hii mara ya kwanza vijiji vitakavyopewa viwe pilot, lakini kila Jimbo lazima liwe na kijiji au kimoja au viwili ili tujue kila Jimbo performance ya mpango huu unafananaje, vinginevyo …
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naunga mkono hoja.