Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hotuba nzuri ya Waziri wetu wa Maliasili na Utalii, ambayo hakika kwangu imetoa fumbo au imetoa jibu la mambo ambayo nilikuwa nahitaji kuyasikia. Mheshimiwa Waziri kwanza nikupongeze na kukuunga mkono katika hotuba yako hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yote naomba kumwambia ndugu yangu Msigwa nimemsikia hapa amezungumza juu ya jambo la Green Miles. Ninachokifahamu Mheshimiwa Msigwa, hukumu imeshatolewa juu ya kesi ile ya Green Miles. Bahati mbaya sana hawa ambao wewe unaowasema ni dhaifu, hawana sifa, mahakama imeamua kuwapa kitalu. Mheshimiwa Waziri atakuja kuyazungumza vizuri, lakini nilitaka nitoe taarifa hii mapema ili upate kuifahamu halafu Mheshimiwa Waziri aje kututhibitishia kama niliyoyasikia mimi ndivyo yalivyo au yana walakini katika lolote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo, niungane na ndugu yangu Mheshimiwa Msigwa aliposema kwamba nchi hii ni ya kwetu wote na tunapaswa kuzungumzia interest za nchi kwa pamoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Tanzania, mwezi Oktoba mwaka jana, walichagua Chama cha Mapinduzi, tuzungumzie maslahi ya nchi hii. Huo ndiyo wajibu wetu wa kwanza kama Wabunge tunaotokea ndani ya Chama cha Mapinduzi, kuzungumza juu ya interest za nchi yetu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Msigwa anachofanya ni kutukumbusha juu ya wajibu yetu na sisi tunakushukuru kwa sababu ndiyo wajibu wetu kuendelea kukumbushana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu kwa kipindi kirefu sana imekuwa katika migogoro mikubwa ya wakulima na wafugaji, pamoja na hilo migogoro ya uhifadhi na vijiji vyetu nayo imekuwa ni moja ya donda ndugu. Mimi nimewahi kuzungumza katika Bunge lililokwisha, Bunge la Kumi juu ya matatizo makubwa yaliyopo baina ya watu wa kijiji cha Matipwili, Gongo, Mkange, Manda na Hifadhi ya Saadani. Ziko hatua ambazo zilikwishafanyika kipindi kile cha Mheshimiwa Nyalandu, alikwenda kule akakutana na Wananchi wale, wakafanya mikutano, lakini Mheshimiwa Waziri Maghembe, ambaye hii ndiyo bajeti yako ya kwanza ninaamini kwamba kuna vitu unabidi uvisikie kutoka kwetu Wabunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba yale waliyokubaliana Mheshimiwa Nyalandu na wananchi wangu, mpaka sasa hivi imeendelea kuwa ni kizunguzungu na hakuna majibu sahihi yaliyokwishapatikana. Kwa hiyo, ninachokuomba Mheshimiwa Waziri, unapokuja kujumuisha au kuhitimisha hotuba yako, ni vema jambo hili pia nalo ukalizungumza ili wananchi wangu wa vijiji vilivyotajwa, waweze kusikia kauli yako wewe Waziri mpya wa Wizara hii, ukitoa majibu yaliyo sahihi na jinsi gani tunaweza kukamilisha mchakato ambao ulianzishwa na wenzako waliotangulia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo, nimewasikia watu wengi wakizungumza juu ya matatizo ya ng‟ombe katika hifadhi zetu. Mheshimiwa Waziri, nataka nikwambie mimi ninayo Hifadhi ya Wamimbiki, na yoyote yule anayetaka kusimamia hapa kutetea ng‟ombe wakae ndani ya hifadhi huyo ni adui wangu wa kwanza kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwambieni ndugu zangu, haiwezi kugeuzwa nchi yetu ikawa yote ni sehemu ya kuchunga ng‟ombe, haiwezekani, lazima tuweke mipaka na lazima tu- identify maeneo ambayo ng‟ombe wanatakiwa kwenda kuchungwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Halmashauri ya Chalinze, wananchi wa Tanzania, wananchi wa Bagamoyo, kwa kipindi kikubwa sana wamekuwa wanategemea sana Hifadhi ya Wamimbiki kwa ajili ya kupata fedha za kigeni, lakini pia kwa shughuli za kitalii zilizokuwa zinafanyika katika maeneo yale. Sisi wengine Wamimbiki tunatembea na mguu kuingia kule. Tumekuwa tunashuhudia wanyama wakati tuko wadogo, leo hii Mheshimiwa Waziri, wanyama wale hawapo tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu hata hatuelewi wametokea wapi, wamekaa ndani ya hifadhi ya Wamimbiki, baya zaidi ambalo linafanyika hatulipendi, inakatwa miti, watu wanatengeneza makazi ndani yake, na matokeo yake ni kwamba miezi mitatu iliyopita ndugu zangu tumeshuhudia tembo katika Mji wa Chalinze - Bwiringu. Tumeshuhudia tembo katika Mji wa Chalinze, kwa nini wamekwenda Chalinze, ni kwa sababu hawana njia zingine za kupita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikupeni taarifa kwa sababu sisi wengine kule Chalinze ni kwetu, hatujaenda kutafuta vyeo. Tembo wanapotoka Mozambique, wanakuja kupitia kwa Selous na wakifika maeneo ya Mikumi wanagawanyika katika makundi mawili, lipo kundi ambalo linakwenda Kaskazini mpaka Hifadhi ya Manyara na liko kundi ambalo linakwenda Mashariki mwa Tanzania, ambalo linakwenda mpaka Hifadhi ya Saadani. Kinachoshangaza, kwa shughuli zinazofanyika pale, na shughuli ambazo zinaonekana kwamba Wizara haichukulii kimkakati jambo hili, wale tembo sasa hawana sehemu ya kwenda. Matokeo yake tembo hawa wanatafuta njia nyingine za kufika Saadani, ndiyo matokeo yake wanafika kwenye nyumba za watu na inakuwa ni taabu katika maisha yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili jambo liko serious, hatutakiwi kulifanyia mchezo, kama ambavyo leo hii wako baadhi ya wenzetu kwa mfano, Biharamulo kule, imefika sehemu kwamba wanaomba lile pori sasa ligawanywe ili watu wapate kuhifadhi ng‟ombe, badala ya kufanya shughuli za hifadhi asilia. Kama ambavyo leo hii mbuga ya Serengeti inataka nayo kupotea kwa kuwa ng‟ombe wamejaa wengi au kule katika pori la Kigosi na pori tengefu la Loliondo. Mheshimiwa jambo hilo kwa Halmashauri ya Chalinze hatuko tayari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima leo hii, utuambie ni mkakati gani ambao kama Wizara mnao na mmejipangaje kuhakikisha kwamba mnaondoa mifugo hiyo katika eneo lile ili sasa mambo mazuri ya uhifadhi wa hizi asili uendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo, Mheshimiwa Waziri tunalo tatizo lingine pia katika Uzigua forest; Uzigua forest imekuwa ni kilio cha muda mrefu na mwisho wa siku hapa mzee tunaweza tukageuzwa majina yetu yakawa ni Uzigua forest hapa, Mheshimiwa Waziri hili nalo naomba ulitolee jibu. Wananchi wamekuwa wanauliza juu ya mipaka ya hiyo Uzigua forest, lakini hifadhi yetu hii imeendelea kukua, inaonekana tofauti na ambavyo hifadhi nyingine zinaendelea kuwepo. Lakini majibu yamekuwa ni yale yale kwamba tutakuja halafu hatuna jibu la moja kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, Mheshimiwa Waziri, na hili jambo nafikiri ni jambo la Serikali yote ilisikie. Kumekuwa na tatizo moja la ECO-Energy. ECO-Energy walipewa maeneo na vijiji vyetu, lakini cha kushangaza zaidi baada ya kutangaza juzi kwamba mradi ule hautokuwepo, kipande cha hifadhi ambacho kilikuwa katika miliki ya vijiji vyetu vile, hifadhi ile kinarudishwa katika eneo la TANAPA, Saadani.
Mheshimiwa Waziri naomba tu nikupe angalizo, wananchi wangu wa Halmashauri ya Chalinze, walitoa maeneo yale kwa ajili ya kupata faida nayo. Faida yao kubwa ilikuwa kwamba ECO-Energy walime miwa, lakini wao wawe ni outgrowers. Leo hii maeneo yao yale meamua Serikalini kuyachukuwa na kuyafanya yawe sehemu ya TANAPA. Mheshimiwa Waziri nataka nikwambie, katika jambo hili hatutokubalina na mimi nitakamata shilingi yako kama hakutakuwa na jibu ambalo linatuambia kwamba ardhi hii itarudishwa kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Serikali mnaweza mkaamua lolote, lakini katika jambo hili la ardhi ya wanavijiji wangu, kama hatujafika na sisi kulalamika, kama alivyolalamika juzi Mheshimiwa Mbowe pale na ardhi ile ya Kilimanjaro, ningeomba jambo hili mlitolee majibu mazuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya Operesheni Tokomeza, wenzangu wamezungumza kwamba ardhi ile ya Operesheni Tokomeza imechukuwa bunduki za watu, imechukua magobole ya wazee wangu pale katika vijiji vyetu vinavyozunguka hifadhi zetu, lakini baada ya kumalizika operesheni ile hatuoni silaha zile zikirudishwa kwa wananchi wale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri, uje kutoa jibu katika jambo hili. Mwenzako Mheshimiwa Nyalandu hapa alikuwa kila siku anatumbia kwamba itatoka kesho mpaka anaondoka hakuna jambo lolote. Nataka wewe katika Serikali hii, uje kutuambia inakuwaje juu ya yale mambo ambayo tulikuwa tunaongea kila siku juu ya silaha hizi za jadi walizokuwa wanatumia wazee wangu pamoja na magobole na mambo mengineyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo, nieleze pia kama walivyosema wenzangu juu ya jazba zilizotawala humu ndani!
Waheshimiwa Wabunge, hatupaswi kuwa na jazba! kazi yetu Wabunge ni kushauri, tutumie nafasi hiyo kushauri. Maana leo hii tunaposikia kauli kwamba hii CCM gani, mimi nikiwa kama Mjumbe wa NEC, naomba ni- declare interest, nakwazika...
MWENYEKITI: Ahsante.