Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi. Mimi nianze na Wizara kama ambavyo mchangiaji Mheshimiwa Lucy Owenya amesema, ili tupandishe uchumi wa Southern circuit lazima tufungue milango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba sana Bunge lililopita tumezungumzia sana kuhusiana na uwanja wa Nduli Iringa pamoja na barabara inayotoka Iringa Mjini kwenda National Park. Ningeomba Wizara kama inawezekana hebu tushirikiane basi hata na TANAPA tutengeneze ile barabara kusudi tuweze kuzalisha pesa nyingi zinazotokana na hifadhi ambayo ni kubwa ya pili hapa Afrika, ningeomba hilo mlifanyie kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ninataka nizungumzie kuhusu wanyama waliotoroshwa, hiki ni kiporo. Kwa bahati mbaya Wabunge huwa tunasahau tulikotoka, hiki ni kiporo. Bunge lililopita tumezungumza sana juu ya ujangili, lakini kuna wanyama waliokuwa wametoroshwa uwanja wa KIA. Bunge lililopita tulitoa azimio, AG wewe ni shahidi hapa tulikubaliana wote kwamba lazima ufanyike uchunguzi ni akina nani walitorosha wale wanyama, sasa hivi hakuna kesi, mwanzoni mlikuwa mnasingizia kuna kesi mahakamani, sasa hivi hakuna kesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, iliingiaje ndege ya kijeshi? Jeshi lilionaje hapa? Usalama wa Taifa ulionaje? Hayo mambo bado hayajatolewa majibu. Serikali ya Qatar, nilibahatika kwenda Qatar walisema wamezoea kuchukua wanyama kwa style hiyo. Tulitoa Azimio kwenye Hansard inaonyesha Bunge lililopita. Ninaomba Waziri haya mambo hayawezi kulala kiporo kama tunataka tukomeshe ujangili, maana yake Serikali hii imesema inafukuwa makaburi, tuendelee kufukuwa makaburi hayo ni nani alihusika kutorosha hawa wanyama kuwapeleka Qatar, lazima turudishe na Bunge liliazimia. Naomba AG utasaidia Wizara hii namna gani tulifanye.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu ni hili suala ambalo Kambi ya Upinzani imezungumzia kuhusu Kampuni ya Green Miles. Kampuni ya Green Miles, amezungumza Mheshimiwa Mbunge Mzee wangu hapa, mimi nilkuwa miongoni mwa Kamati ya Wabunge wanne, tuliokuwa tunachunguza utoroshaji wa wanyama. Tulipochunguza kampuni ya Green Miles, kama alivyosema haikupewa vitalu vya uwindaji kwa sababu ilikuwa haina sifa. Kamati ya ushauri ilimshauri Waziri kwamba hii kampuni haina sifa, imesema uongo, lakini haihifadhi kwa sababu kwenye kuwinda kunahitaji uhifadhi, kwa bahati mbaya au vinginevyo mambo yalivyokwenda hii kampuni ikapewa. Ilivyopewa tukayashuhudia yale ambayo walivunja kanuni za uwindaji na kulikuwa na infringement zaidi ya 11.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 4 Julai niliweka CD hapa kuonesha jinsi ambvyo wanawinda vibaya! Hawa watu hawana sifa za uhifadhi na Waziri aliyepita aliamua kuifutia leseni ya uwindaji kwa sababu wanawinda vibaya, suala hili lilivuta hisia za Kimataifa katika masuala ya uwindaji, suala hili lilivuta hisia za Watanzania vituo karibu vyote vya televisheni vilionesha jinsi ambavyo hawa watu wanawinda vibaya wanyama, hawana sifa ya kuwinda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kushangaza Mheshimiwa Waziri umetoa barua tena. Hapa Mheshimiwa Maghembe, kwenya masuala ya uhifadhi niko na wewe, sikubaliani kwamba ng‟ombe waende kila mahali, lakini kwenye suala hili sikubaliani na wewe. Kwa sababu tunakubali kuwa uwindaji ni pamoja na uhifadhi, hunting is about conservation. Mwindaji yoyote ambae hawezi ku-conserve nature hatustahili katika nchi yetu! Sasa inawezekanaje hawa watu ambao hawana sifa, kuna infringement zaidi ya kumi na ngapi? Lakini Waziri aliyekutangulia alifuta, kulikuwa na makosa sita aliyaona. Walikuwa wanawinda ngedere hawaruhusiwi kuwinda ngedere.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtoto wa chini ya miaka 16 anawinda, sheria inakataa, walikuwa wanatumia bunduki ambazo zinaziba sauti, sheria inakataa, wewe mwenyewe unaijua kwenye sheria ya mwaka 2009 na regulations za mwaka 2010. Hawa watu wamevunja sheria, leo wanarudi wanarudi kwa mlango gani? Ninaomba Waziri utuambie hawa watu ambao hawana sifa za kuwinda wamerudije tena kwenye maeneo hayo? Tutakuwa tunaleta mchezo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niwaombe Waheshimiwa Wabunge hebu tuwe consistance kama tunataka tufanye uhifadhi. Wale waliokuja kuchukuwa wanyama wetu, watu walipiga kelele sana Bunge lililopita wakasema tunataka hata mifupa irudi. Nani alichukuwa hao wanyama? Hiyo ndege ya Qatar iliingiaje? Tulizungumza hapa kwamba mpaka na Ikulu ilikuwa inahusika, hatujapata majibu ya kutosha. Lakini hawa ambao walizuiwa wanarudi tena kwa mlango wa nyuma wamerudije? Naomba Mheshimiwa Waziri haya mambo utupe majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine kuna Mbunge, asubuhi amezungumza kwamba mpaka kwenye magazeti wanaandika kwamba kuna Wabunge wengine ni majangili. Hii ni kashfa kwa Bunge, hatuwezi kukaa kimya. Hili Bunge tumeambiwa kuna wala rushwa, Bunge hili wengine wanapiga mtindi, Bunge hili tena tunaambiwa kuna majangili. Tutakuwa na chombo cha umma kipi ambacho haya mambo kama hatuwezi kuyasemea? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu mtu kama kweli imeandikwa Jambo Mills gari yake hii hapa, kama ni kweli lazima tupate majibu na kwa bahati mbaya labda yeye hayupo na inasemekana, taarifa zinasemekana mpaka na gari lingine la Jambo Mills lilikamatwa na pembe za ndovu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama vile halitoshi, huyu mtu kuna leseni moja ya madini na yeye anahusika. Haya madini yako kwenye kitalu kule Meatu ambacho kuchimba madini hairusiwi kwenye hifadhi Waziri unajua Huyu mtu sijui amepataje kulikuwa hakuna EIA? Amepata, wanatumia wafugaji kuwaingiza eneo la uwindaji kwa kisingizio kwamba hawana malisho ili waweke pressure kusudi wakachimbe madini mpaka wamepata hiki kibali.
Nimshukuru Mkuu wa Mkoa alizuia hiki kibali na nimuombe Waziri wa Madini alifuatilie hili suala, ni nani alitoa kibali hiki, watu waingie kwenya hifadhi, sheria yetu inakataa kwamba wasiingie kwenye hifadhi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa huyu kama kweli haya mambo yanafanyika na yeye anahusika, Bunge lijisafishe, tujue kuna tatizo gani kama ni ya uongo asafishike, lakini vyombo vya habari vimeandika, vyombo vya habari vimetoa, anahusika, wanasema kuna Mbunge anahusika wamemtaja kwenye magazeti, ukienda kwenye mitandao na yeye hajakanusha. Lakini kuna wakati walivyokamatwa hawa watu waliachiwa, wakatoa fedha kidogo tu wakati wengine wanasota.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanasafirisha tumbili, umewaweka ndani sasa hivi wanasota, lakini hawa watu wanatembea, inaoneka waliokamtwa wana nasaba na huyu mtu alyetajwa hapa, lakini wametoa faini wakaachwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanyama wanaonekana hapa hawakuchukuliwa hatua zozote, lakini wengine wamesafirisha tumbili tu wale tena wana haki, wale walikuwa wanasafirisha tumbili vizuri hawana makosa, akina Mzee Mlokozi wale wanalala tu kule ndani. Hawa wanatembea barabarani na wanatumia kisingizio, nikuombe hata hili suala la Toya Mheshimiwa Waziri hebu liangalie kwa upana wake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwa bahati nzuri miaka yote mitano nimekuwa kwenye hilo eneo kidogo naelewa, watu wa Toya muwaangalie kwa jicho la karibu sana. Manyanyaso wanayoyapata na taabu wanayoipata kwa kweli haiwahusu. Tunajaribu kuwarudisha nyuma hawa ambao ni Watanzania wazawa, wanafanya biashara zao, tunawa-drag chini bila sababu. Niombe Watanzania wenzangu the fact sisi ni Wabunge hapa, tupo kwa ajili ya maslahi ya Watanzania na Taifa kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna msemo mmoja unasema: „it is not economical to go to bed early and save all the candles if the result is twins (siyo jambo la kiuchumi kwenda kulala mapema ukatunza mishumaa yote kama matokeo yake yatakuwa ni mapacha). Kama tutadhani ni uchumi kupeleka ng‟ombe kila mahali kusiwe na mipaka, tusidhani litakuwa jambo la kiuchumi, baadaye tutapata hasara ya Taifa hili, ni lazima tu-save nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii ni ya wafugaji, nchi hii ni ya wakulima, nchi hii ni ya wafanyakazi, nchi hii ni ya viwanda, kwa hiyo, lazima tutenge maeneo. Ndiyo maana China walivyoona nchi ni ndogo wakaweka sheria ya kuzaa mtoto mmoja. Kwa hiyo, hatuwezi tukasema ng‟ombe wawe kila mahali, hatuwezi kusema ufugaji uwe kila mahali, tukabaliane wote kama viongozi, tutenge maeneo maalum. Mheshimiwa Waziri, kuna asilimia 10 nchi hii ya ufugaji wa ng‟ombe, ambao ng‟ombe tulionao milioni 25, wakiwekwa vizuri tunaweza tukawatunza. Lakini hatuwezi kukubali kutumia mifugo tukaharibu uhifadhi, tukaharibu utalii ambao unatuletea fedha za kigeni asilimia 25 na GDP ya asilimia 17. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, badala ya kugombana hapa na wananchi wametuita hapa kama viongozi, kama watu wenye busara, badala ya kugombana hapa kuwa na mawazo madogo ya kuwaza Jimbo lako hebu tuwe na national interest, tukae wote kwa pamoja tukubaliane. Hii nchi ni yetu sote, tukubaliane mifugo ikae wapi, samaki wakae wapi, ng‟ombe wake wapi? Mheshimiwa Waziri tukiruhusu jazba zitutawale hapa tutaishia kugombana. Kama wananchi huko wakituona, mfugaji anagombana na mkulima, mkulima anagombana na mfugaji, huko nje tutaanzisha vita.