Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia katika Wizara hii muhimu ambayo inachangia Pato kubwa la Taifa. Kwanza kabisa nipende kuipongeza hotuba nzuri ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mchango wangu mimi nitajikita kwenye suala zima la utalii. Tunapozungumzia utalii nitazungumzia mambo matatu muhimu ili tuwe na utalii endelevu. Ili tuwe na utalii endelevu tunahitaji vivutio vya utalii, ili tuwe na utalii endelevu tunahitaji namna ya kufikia vivutio hivyo, tunahitaji malazi ya kuwalaza wageni wetu wanapofika kwenye vivutio vya utalii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza na suala la vivutio vya utalii. Nchi yetu ya Tanzania ni nchi ya pili kwa kuwa na vivutio vyenye ubora wa hali ya juu ukilinganisha baada ya nchi ya Brazil. Lakini cha kusikitisha sana pamoja na kwamba Wizara hii inachangia asilimia kubwa kwenye Pato la Taifa, kwa mfano nikiangalia asilimia 17.5 inachangia Pato la Taifa kupitia Utalii, lakini asilimia 4.8 inatoka kwenye misitu, asilimia 25 ya Pato la Taifa kupitia fedha za kigeni zinatoka kwenye suala zima la utalii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho nashangaa sana tunaona kitakwimu mapato haya ni makubwa lakini ukilinganisha na vivutio tulivyonavyo bado tunahitaji kuwekeza nguvu kubwa sana kwenye suala la kuboresha utalii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na vivutio tulivyonavyo bado tunapata mapato kidogo sana, lakini tunapata watalii wachache sana ambao wanatembelea vivutio vyetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikiliza vizuri hotuba ya Mheshimiwa Waziri, imejaa mambo mengi imejaa mipango mingi; lakini niseme ukweli tusiporekebisha changamoto za miundombinu, hasa miundombinu ya barabara bado suala la utalii tutakuwa tunaimba kila siku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la miundombinu na barabara ni changamoto kubwa hasa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, Mikoa ya Magharibi na Mikoa ya Kanda ya Ziwa. Ukitaka kuwekeza katika Mikoa ya Kusini, Mikoa ya Magharibi na Mikoa ya Kanda ya Ziwa utakumbana na suala zima la changamoto ya barabara. Gharama zinakuwa ni kubwa sana kwa wageni wetu wanaotembelea hifadhi zetu na maeneo yetu ya utalii hii ni kwa sababu ya changamoto za barabara. Wawekezaji wengi wanashindwa kuwekeza katika sekta ya utalii ni kwa sababu ya changamoto ya barabara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia changamoto nyingine kubwa ni ya viwanja vya ndege. Tuna viwanja vya ndege vya kimataifa vya Kilimanjaro, Dar es Salaam, lakini sasa tuna uwanja wa ndege wa Songwe. Uwanja wa ndege wa Songwe ambao tunategemea ndio utakuza utalii wa Kusini hauwezi kufanya kazi peke yake usiposhirikiana na viwanja vidogo kwa mfano kiwanja a Iringa, kiwanja cha Katavi ambacho a ndege zinazokwenda kwenye hifadhi ile ya Katavi zinaweza kutua kule; hatuwezi kukuza utalii wa mikoa hii kama hatuwezi kuimarisha hivi viwanja vya ndege. Nikisema hapa leo gharama ya kutoka Dar es Salaam mpaka kwenye hifadhi ya Ruaha na kurudi ni karibu dola 700, (shilingi 1,400,000).
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ni mtalii gani au mwekezaji gani anaweza kuwekeza kwenye utalii kwa gharama zote hizi? Ni mtalii gani wa ndani ambaye anaweza akatoka mfano Mkoa wa Iringa kwenda Hifadhi ya Ruaha kwa kulipa 800,000 kwa usafiri wa gari? Tutakuwa tunaimba utalii wa ndani, tutakuwa tunaimba uwekezaji lakini hatutoweza kuwekeza kama miundombinu hii haitafanyiwa kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala zima la malazi. Suala la malazi ni changamoto kubwa, niwapongeze wawekezaji wa Mkoa wa Arusha ambao wao wameweza kuwekeza zaidi pia kwenye masuala ya hoteli. Hoteli nyingi zilizopo katika Mkoa wa Arusha zina hadhi za hoteli ya kitalii. Lakini hoteli hizi zinazidiwa wakati wa high season watalii wanalazimika kwenda kulala nchi jirani, wanalala Nairobi ni kwa sababu hoteli hizi hazitoshi, lakini pia hoteli zetu zilizojengwa kwenye mikoa yetu ya Nyanda za Juu Kusini mfano Mikoa ya Iringa, Mbeya, Mikoa ya Magharibi, Mikoa ya Kanda ya Ziwa bado ni changamoto kubwa kwa wageni wanaotembelea maeneo hayo. Kwanza huduma zinazotolewa kwenye hoteli zile ni huduma duni ambazo haziendani na hadhi ya huduma ambazo wageni wetu wanatarajia. (Makofi)
Vilevile ningependa kutoa ushauri kwa Serikali, watoe masharti nafuu kwa wawekezaji hawa mnaotaka kuwekeza katika sekta ya utalii, kuwekeza kwenye tour operators. Kwa mfano mwekezaji anataka kuwekeza Kusini unatofautishaje mwekezaji wa Kusini na mwekezaji wa Kaskazini, kwanza mwekezaji wa Kusini ana changamoto ambazo nimezitaja, vivutio vile viko mbalimbali, barabara ni mbovu, lakini pia mwekezaji huyu hajavutiwa. Wizara haijampa mwekezzaji huyu ya yeye kuwekeza katika mikoa hii ya Kusini. Kwa mfano ukiwekeza katika suala zima la utalii, la tour operator unatakiwa kulipa dola 2,000 na sijui kwa nini ni dola kwa Mtanzania mimi nilitegemea labda watalipa Tanzania shillings lakini analipa dola, dola 2000 kuwekeza tour operator.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu tour operator anahitaji kulipa TRA, anahitaji kulipa SUMATRA malipo yamekuwa ni mengi. Lakini huyu tour operator nitamtofautishaje na tour operator anayekuja kuwekeza Kusini? Wanaokuja kuwekeza Kusini, Mikoa ya Magharibi na Mikoa ya Kanda ya Ziwa wapunguziwe angalau ifike hata dola 1000 ili waweze kuvutiwa kuja kuwekeza katika mikoa ile. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiboresha maeneo haya ya uwekezaji, mahoteli yetu, tour operator, tunaweza pia tukatoa ajira nyingi sana kwa wazawa ambao wengi wamemaliza vyuo. Kwa mfano Chuo cha Taifa cha Utalii kimetoa wanafunzi wengi wa certificate pamoja na diploma tangu mwaka 2006, lakini wanafunzi hawa hawajaajiriwa, hawana ajira hata kwenye Wizara.
Kwa hiyo, ningeomba pia Waziri anapokuja kuhitimisha hapa atuambie pia ni ajira ngapi zimetoka kwa wanafunzi hawa waliomaliza katika chuo hiki kama ilivyo Mweka na Pasiansi?. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ningependa kuongelea suala pia la Maafisa Utalii katika mikoa yetu. Ninaomba Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na TAMISEMI iangalie namna ambavyo itaweza kuajiri Maafisa Utalii kwenye mikoa yetu, wilaya zetu, lakini pia kwenye halmashauri. Hii itasaidia sana kuibua vivutio mbalimbali vilivyoko kwenye mikoa yetu kwa kushirikiana na wataalam. Vilevile itasaidia kuondoa umaskini kwa wananchi wanaozunguka katika maeneo yanayozunguka hifadhi zetu au maeneo yetu ya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wengi wanaoishi kwenye maeneo hayo wamekuwa ni maskini kwa sababu hawana namna ya kutumia vile vituo vyao bila miongozo ya hawa maafisa utalii. Ukiangalia suala zima la utalii wa kitamaduni, utalii huu sasa hivi umepotea hauthaminiwi, lakini ukiangalia nchi nyingi zimekuwa zikitumia utalii wa kitamaduni kuweza kunufaisha wananchi wanaozunguka karibu na maeneo ya hifadhi, wamekuwa wakitumia tamaduni zao, wamekuwa wakitumia taaluma zao kwa mfano wengine wamekuwa ni wachoraji na wameweza kufaidika sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, siungiā€¦