Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabaraza ya Ardhi yanachelewesha kesi hivyo kuchochea migogoro ya ardhi. Kesi inachukua miaka kumi; nini matokeo yake kama siyo kukuza migogoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro kati ya wananchi wa Mwanalugali - Kibaha Mjini na Halmashauri Kibaha Mjini ambao wameporwa ardhi tangu mwaka 2004 kwa madai ya kufidiwa mpaka leo, nini maana yake? Mgogoro kati ya wananchi wa Bagamoyo na EPZ katika shamba ardhi ya Bagamoyo; mgogoro wa ardhi kati ya wafugaji na Vigwaza na wakulima, nashauri wafugaji watengewe maeneo ya mifugo ili kupunguza migogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la CDA ni kubwa. Wafanyakazi wa CDA kupora ardhi za wananchi na kujimilikisha. Mhudumu ana viwanja kumi eti kwa sababu wanapopima wanajipa viwanja na kuviuza kwa bei nafuu. Ushauri wangu ni kwamba mambo ya ardhi yarudi mamlaka ya Mji wa Dodoma. Wananchi wamechoshwa na CDA kwa jinsi inavyofanya kazi kwa maslahi ya wafanyakazi wenyewe.