Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi ya kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Shirika la Nyumba (NHC), Shirika hili lilianzishwa kwa nia njema ya kusaidia wananchi kujenga nyumba za bei nafuu lakini kwa sasa hivi Shirika hili limekuwa ni la kibiashara zaidi. Hivi huko vijijini hata mijini wananchi wa kipato cha chini wawezaje kumiliki nyumba hata ya milioni 30? Ni vizuri NHC wakijenga nyumba wazipangishe kwa bei nafuu na zile kodi zikishalipwa kwa kipindi cha kutosha kulipia deni la ujenzi ndipo mmiliki apewe offer ya kununua nyumba hiyo kwa bei nafuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi zinazotozwa na NHC kwa sasa ni za juu sana na baadhi ya nyumba za biashara hazijakarabatiwa lakini kodi zipo juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua ni master plan ipi inayotumika katika Jiji letu la Dar es Salaam? Wananchi wanajenga kama wanavyotaka, lakini ikumbukwe mifumo ya maji taka ni ile ile iliyojengwa enzi ya mkoloni, wakati huo wakazi waliokuwepo walikuwa ni wachache. Sasa hivi Jiji la Dar es Salaam lina wakazi zaidi ya milioni tano wanatumiaje mitandao ile ile ya kupitisha maji machafu? Je, ni kwa kiasi gani Wizara zinashirikiana ili kutatua tatizo hili? Je, Serikali haioni kwa Jiji la Dar es Salaam haiwezi ni wakati muafaka sasa kusitisha ujenzi wa maghorofa makubwa mpaka pawepo na master plan ili mji ujipange? Hakuna hata viwanja vya wazi, viwanja vya michezo nyumba zinasongamana hata emergency ikitokea katikati ya mji siyo rahisi fire brigade kuweza kupita na kuokoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi za majengo. Kodi hizi ni kubwa sana kwa wananchi wa kawaida kuzilipa, nikiungana na Kambi ya Upinzani, kodi hizi zilikuwa zinakusanywa na Halmashauri na hii ilisaidia sana kuweza kuleta maendeleo katika Halmashauri husika. Ni sababu zipi zilipelekea Serikali kuamua kodi hizo zikusanywe na kupeleka Hazina?