Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaipongeza kwa dhati Wizara katika mikakati yake ya utekelezaji wake wa bajeti ya mwaka 2016/2017. Lengo kubwa la kutaka Serikali kuendeleza ardhi ni kwamba ardhi ni muhimu sana ndiyo inayokuza uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa MWenyekiti, Lindi Manispaa eneo la Mkwaya kuna ardhi kubwa inayomilikiwa na Mhindi mmoja. Ni shamba kubwa haliendelezwi, wananchi wa kijiji cha Mkwaya wanakosa eneo la kulima na mmiliki huyo hafanyi chochote. Ninaiomba Serikali kuona kwa namna gani wananchi wa kijiji cha Mkwaya watasaidiwa kupata ardhi hii ambayo haitumiki waweze kutumia kwa ajili ya kilimo cha mpunga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia moja.