Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya na kwa kunipa fursa siku ya leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri Mheshimiwa Lukuvi kwa kazi nzuri na inayoendana na wakati, lakini la muhimu kwa kuwa muwazi kabisa. Sifa yake imemtangulia. Pia nimpongeze Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu nzuri kwa kazi nzuri na kurudisha matumaini ya Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri maeneo machache ili kuboresha huduma hiyo ya Wizara. Ardhi ndiyo kila kitu, hakuna jambo linaloweza kufanyika bila ardhi, uwazi katika kazi ya Wizara ndiyo mafanikio.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri kwanza Wizara iangalie namna ya kudhamini Halmashauri zetu kupata vifaa vya kupima ardhi na kuandaa hati za kimila. Maeneo mengi nchini ujengaji holela unaendelea kwa sababu ya uwezo wa Halmashauri zetu kutokuwa na vifaa vya kisasa vya kupimia viwanja na miji pamoja na mashamba. Pia vifaa vya ofisini ili kuwa na uwezo wa kutoa hati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii itafanya tupate hati kwa wakati na pia kuongeza mapato ya tozo la ardhi (land rent)kwa kila mtumiaji.
Pia naomba nishauri Wizara iweze kutumia mfumo ule wa kutumia satellite imaging kwenye hati. Pia elimu zaidi itolewe kwa umma juu ya satellite imaging ili kuondoa fidia Serikali inayolipa bila sababu kwa wanaojenga maeneo tunapotaka kujenga miundombinu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze jitihada ya Wizara kumaliza mgogoro. Naomba iunde sheria ya kulinda ardhi ya kilimo bila ya kuwa chini ya mikono ya Halmashauri zetu.