Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwekezaji anayemiliki shamba kubwa Kijiji cha Senzaya amewakosesha wananchi maeneo ya kulima. Eneo analomiliki ni kubwa na ameshindwa kuliendeleza kwa miaka mingi sana. Naomba Mheshimiwa Waziri aingilie kati ili wananchi waweze kurejeshewa eneo la kulima. Jambo baya zaidi ni kwamba sehemu ya eneo hilo lilichukuliwa kinyemela bila kufuata taratibu/sheria za umiliki wa ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia shamba kubwa na NAFCO - Magamba zaidi ekari 12,000 limechukuliwa hivyo wananchi hawana maeneo ya kulima. Ni vyema Serikali ikarejesha sehemu ya shamba hilo ili kuwasaidia wananchi wa maeneo yanayozunguka mashamba hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mashamba yote mawili (Isenzanya na NAFCO) yapo Wilaya ya Mbozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti naomba kuwasilisha.