Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yale niliyochangia kwa kuongea, naomba kwa sababu ya muda haya nayo yaunganishwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imesababisha migogoro ya ardhi katika vijiji vinavyowazunguka. Mipaka ya NCAA iliyowekwa miaka ya 1950 inafahamika na alama bado zipo na pia GN inaonesha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2002 Mamlaka ya Hifadhi ilifanya uhakiki wa maeneo yake na hapo ndipo migogoro ilipoanza. Mamlaka ilichukua maeneo ya wananchi ya kufugia mifugo katika vijiji vya Endramaguang na kijiji cha Lositete bila ya kuwashirikisha wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa NCAA inahakiki mipaka yake kazi inayofanywa na Wizara ya Ardhi. Naomba kutahadharisha kuwa haki itendeke na uhakikiwe mpaka wa zamani na si ule wa mwaka 2002 ambao NCAA walijiwekea. Najua uhakiki huo umelipiwa na NCAA na isije kuwa sababu ya kupindisha haki. Hatutakubali hata mita moja ya ardhi ya wananchi wetu ipotee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna utata wa mipaka halisi kati ya Wilaya ya Karatu na Wilaya za Ngorongoro Monduli na Mbulu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Karatu iligawanywa kutoka Wilaya ya Mbulu na wakati huo mpaka ulikuwa pale juu view point. Eneo la msitu wa Great Northern Forest lilikuwa Mbulu. Baadaye eneo hilo la msitu lilipandishwa hadhi na kuwa msitu ndani ya hifadhi ya Ngorongoro. Hili haliondoi mpaka wa Karatu kuwa pale juu view point. Naiomba Wizara ilete majibu ya mpaka sahihi kati ya Wilaya za Karatu na Ngorongoro na pia kuleta timu ya wataalam ili kuonyesha mpaka sahihi kati ya Wilaya za Karatu na Monduli na pia Karatu na Mbulu.