Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri atusaidie migogoro ya ardhi iliyopo, moja kwenye Bonde la Mwakaleli kati ya TANAPA na wananchi wa Bonde la Mwakaleli katika Kata za Kandete, Luteba na Isange. Tunaomba irudishwe mipaka ya zamani ili wananchi hawa wapate nafasi za kufuga na kilimo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro wa Kyeruku uliopo Kata ya Kisegese, Kijiji cha Ngeleka, kwa sababu shamba hili wananchi wanalihitaji kulilima ili wajikomboe kwenye umaskini na kwa sasa shamba hili lipo tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Busokelo tumetenga maeneo tayari kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za NHC, wananchi hawa wapo tayari kununua nyumba hizo.