Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa fursa hii. Na mimi kwa vile nachangia kwa mara ya kwanza, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata hii fursa, nakishukuru chama changu cha CHADEMA kwa kuniamini na kunipa fursa na nawashukuru wananchi wa Jimbo la Segerea walionipigia kura zaidi ya 49,000. Kwa bahati mbaya sana, nikiwa nimejitoa katika Tume ya Uchaguzi na nimetimiza masharti yote lakini kwa yale yale tunayoyasema kukosa utawala bora, within a deadline, jina langu likarudi nikapigiwa kura zote. Nawashukuru kwa kutupa Madiwani 13 wa UKAWA na tukiwa tumeshinda kwa kura nyingi sana kwa wagombea wote wawili na nawaahidi nitawatumikia, gamba kwetu halina nafasi. (Makofi)
Ndugu Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwenyekiti, kumradhi, mimi ni Mbunge mgeni kwa hiyo nitahitaji sana kujifunza. Nimepitia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 63(2) kinataja wajibu wa Mbunge kwamba ni kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kabla sijaja mahali hapa nilishangaa sana. Je, Wabunge wa CCM kweli huwa wanasoma Katiba? Nini wajibu wetu kama Wabunge? Sisi ni mhimili, kama ulivyo mhimili wa Serikali, kazi yetu ni kuishauri Serikali, kuwaambia tunataka wafanye moja, mbili…
MWENYEKITI: Mimi nawasihi sana Waheshimiwa Wabunge, maana ukisema kwamba huna uhakika na Wabunge wa CCM kama wanasoma Katiba na wewe ni mgeni, sasa umepata uzoefu wapi? (Makofi)
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nimepata uzoefu kwa kuangalia kwenye television kwamba hatutimizi kazi yetu ya msingi ambayo ni kuishauri Serikali. Mimi ndiyo nachoenda kufanya, kuishauri Serikali. Sipo hapa kwa kazi ya kuisifia Serikali, sipo kwa kazi ya kumsifia Magufuli kwa sababu aliomba kura mpaka kwa kupiga push-up, kwa sababu alijua jukumu analoenda kufanya. (Makofi)
Tumekuwa na changamoto ya ardhi. Nimepitia Mpango na mnaonyesha takwimu zenu kwamba kwa nchi ya Tanzania, mmeweza kupima 10% tu ya ardhi ya Tanzania. Natokea katika Jiji la Dar es Salaam ambalo limekuwa na migogoro mikubwa ya ardhi. Wananchi zaidi ya kaya 16,000 zimewekewa alama ya “X” kwamba wanaishi kwenye mabonde, wanaenda kubomolewa majumba yao. Zaidi ya watu 99,000 watakuwa ni watu wasio na makazi. Changamoto ni kwamba Serikali ilikuwepo, watendaji walikuwepo, Waziri Lukuvi ambaye ni Waziri sasa alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alifanya nini wakati wote ambapo wananchi wameishi katika maeneo hayo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka mwaka 1998 yalitengwa maeneo ya Tegeta ili wananchi waliokuwa wanaishi mabondeni wahamie hali kadhalika mwaka 2011 akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Wananchi wa Jimbo la Segerea, wananchi wa Ilala, wanataka viwanja vyao kwa sababu wanasema anahusika katika uporaji wa maeneo waliyopewa wananchi waliokuwa wanaishi mabondeni. Kama hiyo haitoshi, tuna changamoto ya migogoro ya ardhi kwa sababu Wizara ya Ardhi haijafanya kazi. Kuna migogoro ya wakulima na wafugaji kwa sababu asilimia kubwa ya maeneo hayajapimwa. Alivyochaguliwa au alivyoteuliwa juzi, pale katika Wizara ya Ardhi kulikuwa na National Council of Professional Surveyors, ni Bodi ya ma-surveyor, ameenda pale akaivunja. Pengine alifanya kitu cha msingi lakini tokea ameingia katika huo wadhifa amefanya nini baada ya kuvunja hiyo Bodi ambayo ilikuwa inashiriki katika kukagua na kudhibiti wanavyofanya kazi ma-surveyors? Tunaendelea kutengeneza migogoro juu ya migogoro. Tunafanya kazi kwa kutafuta sifa. Tumekuwa watu wa hapa kazi tu na tunafanyia kazi kwenye TV. Mawaziri wanashindana nani leo ataonekana kwenye media, hapa tuwashauri mfanye nini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wengine ni ma-celebrity wazuri tu. Katika kitabu cha Ideal State, Plato aliainisha makundi ya aina tatu. Kuna iron, silver na golden. Kuna wengine walipaswa kuwa ma-celebrity leo ndiyo tumewapa Uwaziri na tunawapa dhamana kubwa ya kuongoza Serikali. Tunakosa cha kuwashauri kwa sababu kila mwaka mnakuja na mipango mizuri ambayo haitekelezeki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, narudi kwenye suala la miundombinu hususan Jiji la Dar es Salaam. Mmejipanga kwamba mnataka viwanda lakini viwanda tunaviwekaje katika maeneo ambayo hayana barabara? Unasafirishaje hayo material pamoja na vilivyozalishwa kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine? Ni changamoto ambazo ni za msingi. Segerea hatuna barabara kwani zote ni mbovu na hatuna barabara za mitaa zote ni mbovu. Serikali ipo miaka 54 ya Uhuru na mnataka tuwashauri, tuwashauri nini wakati mmekuwa mnasema kila siku mnashindwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la lingine ambalo nitalizungumzia ni gap baina ya walikuwa nacho na wasiokuwa nacho. Inaonyesha, tangu mwaka 1992 tulikuwa na umaskini kwa asilimia 39 lakini mpaka mwaka 2007 mmeweza kupunguza kwa asilimia nne tu. Miaka 15 mmepunguza umaskini kwa asilimia nne tu na leo mnasema tuwashauri, tuwashauri nini? Tunachoweza kuwashauri, tokeni, mmeshindwa, tunaomba tuweze kuongoza nchi kwa sababu tunastahili. (Makofi/Kicheko)
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nazaliwa Mkoa wa Kagera, Wilaya ya Kyerwa, nitawasemea. Nimeenda katika Mkoa wa Kagera, Wilaya ya Kyerwa, nilichokikuta, Waziri wa Mambo ya Ndani aende kuona, kuna watu wamejitangazia nchi ndani ya nchi. Kuna watu wanajulikana kama Runyogote, Daniel na mwingine alikuwa Mbunge katika Bunge hili la Jamhuri, wametangaza nchi yao ndani ya nchi. Wana uwezo wa kuamrisha, wakaamrisha Askari wakaenda kukamata watu, wakakata migomba na wakapiga wananchi. Wanaweza kutangaza tunafunga barabara na wakafunga barabara.
MWENYEKITI: Ahsante sana.