Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwasilisha baadhi ya mambo muhimu ambayo yanatakiwa kupatiwa ufumbuzi wa haraka katika Jimbo la Iramba Mashariki, Wilaya ya Mkalama, Mkoa wa Singida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mkalama imekuwa na changamoto zifuatazo:-
(i) Hatuna Afisa Ardhi Mteule – yupo Afisa Ardhi lakini hajapata uteule, hivyo tunaomba ama tupatiwe Afisa Ardhi Mteule au aliyepo ateuliwe ili shughuli za upimaji ziweze kuanza.
(ii) Wilaya haina Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na tunaomba tupatiwe kwani wananchi wa Mkalama wanapata shida kufuata huduma hiyo Wilaya ya Iramba na kusababisha usumbufu mkubwa wa gharama na muda.
(iii) Migogoro ya mipaka kati ya Wilaya na Wilaya; Mkalama vs Mbulu, upo mgogoro wa mpaka katika Kata ya Mwangeza kijiji cha Iramoto na Kata ya Eshgesh na Mbulu.
(iv) Hali ya usalama ipo mashakani kwa sababu wananchi wa Eshgesh sasa wameamua kujenga shule ndani ya eneo la Wilaya ya Mkalama na watu wa Iramoto hawapo tayari kuona jambo hilo.
(v) Mgogoro wa ardhi Mkalama vs Hanang, jiwe la mpaka kati ya Wilaya hizi mbili limewekwa katikati ya kijiji cha Singa “B” Kata ya Hilbadau, jambo ambalo limezusha mgogoro mkubwa na manung‟uniko kutoka kwa wananchi wa Wilaya ya Mkalama.
(vi) Mkalama vs Singida Vijijini katika eneo la Kata ya Kihonda wananchi wa Singida Vijijini wameamua kujenga shule ndani ya Wilaya ya Mkalama hivyo kuhamisha mpaka bila idhini ya mamlaka husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna migogoro ya ndani ya Wilaya, baadhi ya migogoro hiyo inayohitaji Wizara iingilie ni hii ifuatayo:-
(i) Shamba la Mifugo la Makomoti, mipaka ya shamba hili inadaiwa kupanuliwa/kuongezwa bila idhini ya vijiji husika na baadhi ya wananchi wamejenga ndani ya mipaka mipya na wanalima, hivyo kuanzisha mgogoro mkubwa, vijiji husika ni, Ishenga, Kihonda, Kinyangiri. Tunashauri Wizara iingilie na wataalam wa Wilayani wasihusike kwani wanadaiwa kuwa na maslahi binafsi na eneo hilo.
(ii) Kijiji cha Iramoto kilichopo Kata ya Mwangeza yupo mwekezaji kwa jina la Mr. Afrika ambaye anapewa ekari 700 ambazo ndani yake kuna Kaya 80 hivyo wananchi wanalalamika.
(iii) Kijiji cha Msiu, Kata ya Mwanga yupo mwekezaji anayedaiwa kuwa na haki ya kupewa ekari 200 lakini amehodhi ekari 500 na mahakama imeshindwa kwa makusudi kutoa hati ya mwekezaji huyu kuja kupewa ekari 200 anazostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii. Naunga mkono hoja.