Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza uteuzi wa Waziri na Naibu Waziri kwa Wizara hii na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kwani ni watendaji wenye weledi mkubwa kwa kujituma kwao na kujitoa kwao katika kupatikana utatuzi wa mambo yanayowakera wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kuendelea kujipanga na kuandaliwa sheria maalum ya kuwawezesha wawekezaji kutoa mchango wa maendeleo ya huduma za jamii kwenye vijiji vinavyomzunguka hilo liwe mojawapo ya sharti maalum kwa mwekezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto zinaongezeka ndani ya Wizara hii kwenye maeneo yetu ya vijiji, miji na majiji ni upungufu wa watumishi ukizingatia hadi sasa ni asilimia 24 tu kati ya mahitaji yanayohitajika kuanzia Halmashauri hadi Wizara. Ushauri kwa Serikali ni uwepo uthibitisho wa kuthubutu kuongeza ajira na matumizi ya vitendea kazi vya kisasa vinavyoendana na mtandao wa dunia. Angalau kwa asilimia 50 ya watumishi, wanaohitajika tupate ufanisi katika nyanja zote na tuepukane na migogoro iliyokithiri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wamekuwa na migogoro ya wawekezaji na vijiji, panaposhindikana kulipwa kwa fidia ndani ya muda wa uthamini, ni vema Serikali kuona mwelekeo wa kuwapimia wawekezaji nje ya maeneo ya wananchi kwani wao wana uwezo wa kuweka huduma zote za jamii, popote watakapowekwa kuliko kuwachanganya wananchi na kuwazorotesha maendeleo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, muhimu kuliko yote na kuwezesha yote yaliyopangwa kutekelezwa ni kuhakikisha fedha zilizopangwa kutolewa kwa wakati na katika ukamilifu kama Bajeti iliyopangwa na kuidhinishwa na Bunge hasa shilingi 20,000,000,000 kwa miradi ya maendeleo, kwa nini tumekuwa na viporo vingi vya miradi ndani ya nchi yetu ambayo inawadhoofisha wananchi. Ingawa kiasi hicho hakitoshelezi kwa maendeleo ya jumla kwa Wizara hii. Naomba kuwasilisha.