Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na umuhimu wa Wizara ya Ardhi napenda kushauri mambo yafuatayo ili kuepukana na migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara katika Mkoa wa Rukwa na nchi nzima kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabaraza ya Ardhi yaboreshwe kulingana na utendaji wanapokuwa katika Mabaraza ya Ardhi. Kutokuwa na elimu ya kutosha kumepelekea kupata migogoro mingi katika Halmashauri zetu. Hati za kimila, mara nyingi zimekuwa hazitambuliki kwa baadhi ya watendaji katika Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Manispaa ya Sumbawanga iliyopo katika Mkoa wa Rukwa na Wilaya zake, kata na vijiji pamoja na mitaa na vitongoji vyake. Serikali ina mkakati gani wa kuwapa semina watu hawa ili kuondoa migogoro, kuwawezesha Maafisa Ardhi, kwa kuwapa vitendea kazi. Maafisa Ardhi hawa wamepelekea migogoro mikubwa sana katika Halmashauri zetu kwa kutomaliza mogogoro kwa wakati na mahali pengine kutokea migogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro kati ya wawekezaji na wananchi, kulingana na migogoro hii kutokea kila eneo katika nchi yetu, nashauri Serikali kutafuta njia sahihi ya kumaliza migogoro hii ya wawekezaji na wananchi kwa kuweka njia shirikishi kuanzia ngazi ya chini ili kuboresha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro kwa wananchi wa Isesa na mwekezaji, huu ni mgogoro wa muda mrefu uliopo katika Manisapaa ya Sumbawanga Mjini na Vijijini, suala hili limechukua muda mrefu hata kwenye kitabu cha Waziri mgogoro huu haupo, naomba Wizara ichukue hatua haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la fidia kutokuwa wazi, kutokuwalipa wananchi fidia kwa muda muafaka inapelekea migogoro mingi katika Halmashauri zetu kutokana na taarifa tufauti na kupelekea migogoro isiyo ya lazima, nashauri Serikali kutoa fidia kwa wananchi na kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kutoa hati kuchukua muda mrefu, kutokana na hali hii kushamiri hasa katika Mkoa wa Rukwa, Manispaa ya Sumbawanga na ili kuondoa tatizo hili Serikali imegundua tatizo hili, imegundua ni nini linalochelewesha? Pia migogoro kati ya wakulima na wafugaji nashauri Serikali kupima maeneo nchi nzima ili kuepukana na tatizo la migogoro inayoendelea na kupelekea vifo mbalimbali vinavyotokana na migogoro hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi ya ardhi katika Manispaa ya Sumbawanga kulingana na suala hili kuwa na hali ya kutokuwa na usimamizi mzuri wenye uwazi ili kuondoa migogoro isiyokuwa na tija. Suala la ushirikishwaji ngazi za mitaa, hali hii ya kutokushirikishwa hasa kupewa ramani na kuyajua maeneo ya wazi ili kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza bila sababu.